"LET THERE BE LIGHT" Ministries
home  |  Kenyan Booklets

KUBADILISHA  MALAIKA  WATATU



Chapa ya Kwanza, 2001 (Kiingereza)

Copyright © 2001 held by

“LET THERE BE LIGHT” MINISTRIES (rs)
P. O. BOX 328,
Rogue River, OR  97537
U.S.A.

     Haki zote zimehifadhiwa. Ruhusa imetolewa kukichapisha kijitabu hiki, ikiwa tu kitatolewa kama kilivyo bila mabadiliko au maoni.



     Kwa kupata vijitabu vingine zaidi, na hata kupata orodha yote ya vitabu na majarida, tafadhali tuandikie:


Endtime Glorious Message,
P.O. BOX 280,
OGEMBO, KENYA,
EAST AFRICA.

AU

Booklets
P.O. BOX 328
ROGUE RIVER, OR  97537
U.S.A.




KUBADILISHA  MALAIKA  WATATU

     Ujumbe wa malaika Watatu umebadilishwa ambayo ni hatua ya uasi. Neno “Kubadilisha” humaanisha “kugeuza asili, umbo, au ubora” kutoka katika kilichokusudiwa awali. Hivyo, “Kubadilisha Malaika Watatu” humaanisha kugeuza ujumbe wa awali wa Ufunuo 14 katika asili, umbo, au ubora kwenda katika ujumbe mwingine kabisa.
     Malaika ni roho (Ebr 1:7, 14; Zab 104:4). Malaika watatu wa Ufunuo 14 wanahusika na ujumbe kutoka mbinguni, hivyo ni malaika wa haki au watakatifu (au roho). Lakini kuna roho zingine zilizoorodheshwa katika Ufunuo 16 ambazo zinahusika na ujumbe kutoka kwa Ufalme wa Shetani, hivyo siyo roho za haki bali roho chafu. Ni ujumbe tu kutoka kwa malaika watatu wa Ufunuo 14 – ambao umejikita katika Yesu, au ni ujumbe wa roho tatu za Ufunuo 16 – uliojikita kwa Shetani, ambao utasikika na kupokelewa na dunia leo. Kwa hiyo ikiwa ujumbe wa mbinguni wa malaika watatu wa Ufunuo 14 umebadilishwa kutoka katika ukweli uliokusudiwa, basi hautakuwa ukweli tena, lakini utakuwa sehemu ya ujumbe wa kuzimu wa roho tatu za uchafu za Ufunuo 16.     Pamoja na hayo ni nani angefanya hivyo? Nani angejaribu kubadilisha ukweli huu wa thamani wa Mungu katika ujumbe wa madanganyifu ya Shetani kutoka katika shimo la kuzimu?
Katika “Selected Messages”, kitabu cha 1, ukr. 204-205, tunapata kauli iliyovuviwa:
     “Adui wa roho amejaribu kuleta kile kinachodhaniwa kwamba ni uamsho mkuu ambao ungetokea kwa Waadventista Wasabato, na kwamba uamsho huu ungefuatana na kuacha mafundisho yaliyo mihimili ya imani yetu, na kujihusisha na kitendo cha kulipangilia upya Kanisa. Kama uamsho huu ungetokea, nini kingetendeka? Kanuni za ukweli ambazo Mungu katika hekima yake amelipatia Kanisa la Masalio zingeachwa. Dini yetu ingebadiliswa. Kanuni za lazima ambazo ndizo zimelitegemeza Kanisa katika kazi yake kwa miaka hamsini sasa zingehesabiwa kama makosa. Jumuiya mpya ingesimamishwa. Vitabu vya mpango mpya vingeandikwa. Mfumo wa falsafa za akili ya kidunia ungeletwa Kanisani. Waanzilishi wa mfumo huu wangeenda mijini, na kufanya kazi kubwa na ya ajabu. Sabato, kwa hakika, ingechukuliwa bila uzito, hali kadhalika na Mungu aliyeiumba. Hakuna ambacho kingeweza kusimama kinyume na mfumo mpya. Viongozi wangefundisha kwamba wema ni bora zaidi kuliko kosa, lakini Mungu akiwa ameondolewa, wangeweka mategemeo yao katika nguvu za mwanadamu, ambaye, bila Mungu, ni bure. Msingi wao ungejengwa kwenye mchanga, tufani na dhoruba ingetowesha jengo.
     “Nani ana mamlaka ya kuanzisha mfumo kama huo? Tunazo Biblia zetu. Tunao uzoefu wa maisha, uliojaribiwa kwa utenda kazi wa Roho Mtakatifu. Tunao ukweli ambao hauruhusu mapatano na dunia. Je, hatutakataa kila kisichoendana na ukweli?”

     Ellen White aliandika kwamba kungekuwepo na uamsho wa kishetani na mchakato ndani ya Kanisa la Waadventista Wasabato ambao ungejumuisha kutupilia mbali mafundisho ya awali na mihimili ya Waadventista, na hivyo “dini yetu ingebadilishwa.”
Mungu aliinua Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) kutoka katika kukatishwa tama kwa hali ya juu kulikotokea Oktoba 22, 1844, ili kuendelea kuhubiri Ujumbe wa Malaika Watatu ulimwenguni mpaka Kristo ajapo.  Hii ina maana kwamba msingi pekee wa kuwepo kwa Kanisa la SDA ungekuwa Ujumbe wa Malaika Watatu, na utume wake pekee katika siku hizi za mwisho ungekuwa kutangaza ujumbe huu wa mbinguni!
Kanisa la SDA la leo linakubaliana na hili.
     “Nini sababu ya kuwepo kwa Kanisa la Waadventista Wasabato? Kwa kifupi, ni kutangaza kwa ulimwengu mzima injili katika mlengo wa ujumbe maalum wa malaika watatu [Ufunuo 14] na hivyo kuandaa watu kwa ajili ya ujio wa Kristo.” “Adventist Review, August 19, 1982, ukr. 13 (angalia pia “Ministry,” Desemba, 1992, ukr. 24).

     Kutokana na kwamba msingi pekee wa kuwepo kwa Kanisa la SDA ni Ujumbe wa Malaika Watatu, ikiwa Kanisa la SDA lingebadilisha mihimili ya mafundisho ya msingi ya awali ya ujumbe huu katika kitu kingine tofauti kabisa, basi lisingekuwa Kanisa lile lile ambalo Mungu aliliinua. Lakini Kanisa lingekuwa kinyume kabisa na Kanisa la kweli la Mungu.
     Ikiwa hili litatokea, basi msingi pekee wa kuwepo kwa Kanisa la SDA katika siku hizi za mwisho ungekuwa ni kinyume kwa kuleta ujumbe wa roho tatu za mafundisho ya kishetani, na utume wake pekee ungekuwa kutangaza mafundisho haya potofu! Kwa hali hii, Kanisa la SDA lisingekuwa tofauti kama yalivyo Makanisa mengine yaliyoacha nuru ya mbinguni. Hivyo, mwitikio kwa Kanisa hili unatakiwa kuwa kama ulivyo mwitikio kwa Makanisa mengine ya Babeli.
     Kwa hiyo swali kubwa ni: “Je, Kanisa la SDA limebadilisha mihimili ya awali ya mafundisho ya lazima na misingi ya mafundisho ya Ujumbe wa Malaika Watatu wa Ufunuo 14 kwenda katika ujumbe wa malaika watatu wa mafundisho ya kishetani?” Robert Folkenberg, Rais Mstaafu wa Baraza Kuu la Waadventista Wasabato, anaeleza:
     “… ukweli, kama tunavyouelewa katika wakati huu wa mwisho, ni dhahiri, ni wa lazima, unajitetea, utastahimili mtihani wa kupimwa.” Robert Folkenberg, kutoka katika ‘tape’ ya Maswali & Majibu ya maongezi yenye kichwa “Issues and Interviews,” yaliyoandaliwa na Don Snyder [Rais wa Northern California Conference], Februari 19, 1993 kutoka saa 8:00-10:00 usiku katika KCDS, kituo cha redio cha SDA kilichopo Angwin, California, U.S.A.).

     Hebu na tuchunguze na kutumia “mtihani wa kupimwa” katika misingi ya imani na mafundisho ya Kanisa kuona ikiwa “wanaielewa” kuwa bado ni ile ile kama ilivyokuwa misingi ya imani ya awali. Au kama “wanaielewa” kuwa tofauti, na wameibadilisha katika ujumbe potofu wa roho tatu za kishetani.
     Katika kuonyesha kama Kanisa la SDA limebadilisha msimamo wake katika kuelewa Ujumbe wa Malaika Watatu, tutakuwa tunanukuu hasa kutoka katika machapisho, majarida ya Wasabato na hata kauli za viongozi mashuhuri wa Kisabato.
     Wengine wataanza kubishi kwamba vitabu mbalimbali vya Wasabato [SDA] au makala katika majarida ya Kanisa, ambayo yamechapishwa katika mitambo ya uchapaji ya Kanisa, hubeba maoni tu ya waandishi na siyo mamlaka ya Kanisa la SDA kama dhehebu isipokuwa iwe imeelezwa. Lakini hii si sahihi!
     Kulingana na vitabu vilivyoandikwa kutoka katika mitambo ya uchapishaji ya SDA:
     “Mitambo ya uchapaji ya Waadventista Wasabato, iliyojengwa kwa uwekezaji wa dhehebu, haikuimarishwa kwa ajili ya kuchapa chochote kile ambacho mtenda kazi angechagua, lakini kutoa vitabu safi vinavyoweza kutoa ujumbe wetu muhimu ili uweze kuenea kwa upana zaidi katika sehemu zinazoweza kuwakilishwa.
     “Nyumba zetu za uchapishaji…ni watenda kazi katika ujumbe wa malaika watatu – hufanya kazi na kulinda dhehebu lenyewe, mchapishaji wa dhehebu, na mwandishi wa dhehebu. Zote zina jina la dhehebu ili kulilinda, na pia jina la mchapaji na sifa zake kwa kusudi hilo hilo la kumlinda. Kwa hiyo, zina, kamati za vitabu ili kusoma, kutathmini, na kupendekeza hatua maalum ya kuchukua na kuboresha vitabu tarajiwa. Zina Bodi ili kutoa uamuzi wa mwisho, wafanyakazi wenye ujuzi kukagua, kuhariri, na kusahihisha nakala, na kuiweka katika hali inayokubalika….
     “Wakati toleo linapokamilika hubeba muhuri wa mtambo husika unaochapisha, hubeba ukubali wa dhehebu. Hivyo basi, toleo hilo ni la dhehebu, siyo la binafsi. Lina uzito wa mamlaka na hadhi ambayo isingewezekana bila hivyo.” “Ministry,” Desemba, 1948, ukr. 23, Review and Herald Publishing Association.

     Kwa hiyo vitabu vya SDA vilivyotungwa hubeba ukubali wa dhehebu, na ni machapisho ya dhehebu kwa sababu vimechapishwa katika mitambo ya uchapaji ya dhehebu. Hii itabeba ukweli huu huu kuhusiana na majarida na magazeti yote ya Kanisa ambayo pia huchapishwa katika mitambo ya uchapaji ya dhehebu.
     Lakini hasa, hivi vyote vimefafanuliwa ili kuwa msemaji wa Kanisa la SDA: Programu za Sauti ya Unabii, na hali kadhalika gazeti la Voice of Prophecy News, na Signs of the Times. Hivi ndiyo “wawakilishi wa Kanisa la Waadventista Wasabato” (“Eternity Magazine” Septemba, 1957, katika kunukuu misimamo iliyoelezwa ya viongozi wa Kanisa la SDA).
     Siyo majarida haya tu, lakini hasa Adventist Review. Adventist Review linaitwa “Sauti ya Kanisa, kwa ajili ya Kanisa” (“Adventist Review,” Januari 20, 1983, ukr. 8). Mwenyekiti wa Bodi yao ni Rais wa Baraza Kuu (“Adventist Review,” Januari 20, 1983, ukr. 8), na kwa hiyo Review “limekuwa jarida lisilotenganishwa na Kanisa. Katika miaka yote limeeleza hadithi ya Kanisa, na bado linaendelea kufanya hivyo” (“Adventist Review,” Oktoba 24, 1985, ukrasa wa nyuma). Mbali na haya, Review lilikuwa linaitwa “Sauti ya Kanisa la Waadventista Wasabato” (“Review,” May 19, 1966, ukrasa wa mbele).
     Itakuwa ni katika haya majarida matatu ya Kanisa na vitabu kutoka katika mitambo ya uchapishaji ya Kanisa ambayo italeta hitimisho kuona kama Kanisa la SDA limebadilisha msimamo wake wa Ujumbe wa Malaika Watatu au la. Tutaeleza kwanza misingi ya awali ya imani iliyowekwa na waasisi na kufuatwa kama inavyoonyeshwa katika Maandiko ya Ellen G. White, na hatimaye kuonyesha kama Kanisa bado linafuata misingi hiyo tu, au kama limeibadilisha katika ujumbe wa kishetani.


UJUMBE WA MALAIKA WA KWANZA

     “Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, akisema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.” Ufu 14:6-7.

     Injili ya milele ni “Habari Njema” juu ya Yesu na mpango wa ukombozi na wokovu kutoka dhambini kwa njia ya imani katika Yesu Kristo – daraja linalounga kati ya Mungu na mwanadamu (Yoh 14:6; Mwa 28:12-13). Injili ya utukufu hutangaza kwamba tunaweza kupatanishwa na Mungu pasipo gharama (Isa 45:25; Rum 3:28; Gal 2:16; Rum 3:24; Tito 3:7; 1 Kor 6:11; Rum 5:9; 3:4; Mt 12:37; Rum 2:13; Yak 3:20-24), kupokea neema na nguvu ya kusimama (Rum 5:1-5; Efe 6:10-18; Gal 5:1), kupigana na kushinda majaribu na dhambi (Rum 8:1-2) katika haki (Rum 6:16; 5:21) na mwendelezo wa utakaso kwa njia ya Kristo na Roho wake Mtakatifu (Yer 23:6; Isa 61:10; 1 The 4:3-4; 2 The 2:13) anayetutia nguvu (Flp 4:13). Injili hii siyo “imani yote” au “neema yote” ambayo inafunga jitihada zetu, wala siyo “kazi zote” ambazo zinamfungia nje Yesu. Ni kuunganisha utenda kazi wa Uungu na ubinadamu – Mungu akitenda kazi na sisi tukitenda kazi kwa ajili ya wokovu wetu (Flp 2:12-13; Ufu 22:14).

     Maswali kadhaa yanajibiwa na ujumbe wa injili hii, kama:
     – Je, mpango wa Ukombozi na Wokovu ni upi?  Ni tendo “linalotegemea” (“Testimonies for the Church,” vit 2, ukr. 691, vit 5, ukr. 692, vit 3, ukr. 481, vit 1, ukr. 440; “Patriarchs and Prophets,” ukr. 431; “SDA Bible Commentary,” vit  7, ukr. 931) ambapo wanadamu walioanguka wanaweza kupatanishwa tena na Mungu (“Patriarchs and Prophets,” ukr. 331) kwa kufanya kazi kwa ushirika na kuungana na Mungu (“Acts of the Apostles,” ukr. 482; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 372, vit 4, ukr. 464; “Evangelism,” ukr. 596; “The Desire of Ages,” ukr. 296-297) katika kutunza Sheria zake (“Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 218, 225; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 515), na katika kushinda kila dhambi katika maisha yao kwa njia ya msukumo wa matakwa yao (“Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 82; “The Desire of Ages,” ukr. 311; “Steps to Christ,” ukr. 15; “Patriarchs and Prophets,” ukr. 248; “Thoughts from the Mount of Blessing,” ukr. 61; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 513; Mt 11:12; “SDA Bible Commentary,” vit 1, ukr. 1095-1096) kuakisi haki ya Mungu na kutetea tabia yake kwa watu wote (“Patriarchs and Prophets,” ukr. 68). Yesu alifanya mpango huu uwezekane kwa kuzaliwa na bikira, kuuvalisha uungu wake na kuwa mmojawapo wa wanadamu (“The Desire of Ages,” ukr. 363), kwa kuchukua asili ya mwanadamu aliyeanguka juu yake (“Fundamentals of Christian Education,” ukr. 408; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 235; “The Desire of Ages,” ukr. 49, 117; “SDA Bible Commentary,” vit  4, ukr. 1147; “Review & Herald,” vit 1, ukr. 140; vit 3, ukr. 421; “Spirit of Prophecy,” vit 2, ukr. 39), na halafu kushambulia majaribu makuu ya adui kwa njia ya mvuto wa ndani kuelekezwa katika dhambi, lakini bila kuanguka katika hili (“Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 177; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 929; Ebr 4:15; “Signs of the Times,” vit 3, ukr. 264). Hii ilikuwa ni muhimu ili Kristo apitie dhiki na kushinda majaribu makubwa ambayo Shetani huwajaribu wanadamu walioanguka, na hivyo Kristo alivunja nguvu za Shetani kwa mwanadamu (“Prophets and Kings,” ukr. 586), na akampatia mwanadamu mfano kamili na kielelezo cha kufuata katika kushinda pia (Ufu 3:21; “Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 45, 86;  “The Desire of Ages,” ukr. 49; “Sons and Daughters of God,” ukr. 23; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 925, vit 5, ukr. 1082; “Acts of the Apostles,” ukr. 531; “Ministry of Healing,” ukr. 180-181).
     Kristo kamwe hakutumia nguvu zake za uungu alipokuwa duniani (“Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 45; “Counsels to Teachers, Parents, and Students,” ukr. 276-277; “The Desire of Ages,” ukr. 119; “SDA Bible Commentary,” vit 5, ukr. 1124), si hata kwa wengine (malaika walifanya miujiza – “The Desire of Ages,” ukr. 143), lakini kwa ukamilifu alifanya na kumtegemea Baba yake kama msaada wa kushinda majaribu makubwa na kumtegemeza katika kazi yake (“The Desire of Ages,” ukr. 24, 147, 674-675; “Education,” ukr. 80; “Messages to Young People,” ukr. 58). Hivyo Kristo hakuwa na nafasi ya pekee kuwazidi wanadamu wengine, na tunaweza, kwa kuungana na Mungu kupitia Kristo kwa imani, kutumia nguvu zile zile ambazo Kristo alikuwa nazo ili kuishi maisha safi yasiyo na doa katika upendo wa Mungu (“The Desire of Ages,” ukr. 24, 664). Kristo alibeba, akateseka, na kufa juu ya msalaba wa kikatili, akafufuka siku ya tatu, na akapaa mbinguni kuhudumu kama Kuhani Mkuu mbele za Mungu ili kumpatia mwanadamu nafasi ya kumtumikia Mungu au Shetani. Hivyo “ubinadamu wa Kristo una maana ya kila kitu kwetu” (“Our High Calling,” ukr. 48), kwa sababu kama Kristo asingechukua juu yake asili yetu ya kuanguka katika dhambi, lakini angekuwa na asili ya Adamu kabla ya kuanguka au ya malaika, ndipo basi asingeteseka kwa kujaribiwa, na asingejua kile ambacho wewe au mimi tunakipitia pindi tunapojaribiwa. Hivyo asingejua jinsi ya kutusaidia kutoka majaribuni! Lakini Mungu asifiwe kwani sivyo ilivyo. Kristo alikuwa na asili ya kuanguka kwetu katika dhambi juu yake, na aliteseka kwa kujaribiwa. Hivyo aweza kutusaidia katika saa yoyote ya uhitaji (Ebr 2:10, 16, 18, 5:7-9; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 177).

     – Dhambi ni nini? “Dhambi ni uasi wa sheria” ya Mungu, au amri kumi (1 Yoh 3:4; 2:7; Kut 20:1-17).
     – Kupatanishwa ni nini? Kupatanishwa au kuhesabiwa haki ni karama kutoka kwa Mungu ya msamaha wote na kamili kutokana na kukubali, kutubu, na kuacha dhambi (Mit 28:13; 1 Yoh 1:9, “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 391; “SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1071). Kupatanishwa kunadhihirishwa kwa kubadilika tabia (“SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1071), na hakutolewi au kumilikiwa wakati tukivunja amri za Mungu (“Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 213, 366; Yak 2:24). Si kwamba “ukishaokolewa basi utaendelea kuwa umeokoka!”
     – Utakaso ni nini? Utakaso ni kuendelea kukua katika neema (“SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 947) kwa kujifunza kila siku neno la Mungu (1 Kor 6:11; 1 Tim 4:5; Yoh 17:19) na kufa kila siku katika mambo ya ubinafsi na kutembea sawa sawa na mapenzi ya Mungu (“Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 299). Tunapaswa kutunza amri za Mungu ili kufikia na kuendelea katika utakaso (“Counsels on Health,” ukr. 69; “The Great Controversy,” ukr. 467; “Testimonies for the Church,” vit 2, ukr. 472). Hivyo, inamaanisha upendo kamili, utii kamili, kutembea kikamilifu sawa na mapenzi ya Mungu (Isa 5:16; 1 The 4:3-4; 2 The 2:13; “Acts of the Apostles,” ukr. 565).
     – Ina maana gani “kumcha Mungu”? Kumcha Mungu humaanisha kumpenda (Kumb 10:12), kumwogopa (Zab 89:7), kumtumaini (Zab 115:11), kumtumikia (Yos 24:14; 1 Sam 12:14, 24), kumtaraji (Zab 33:18-22; 147:11), kutunza amri zake (Kumb 31:12-13, 17:19, 5:29; Zab 112:1), na kutoka katika uovu (Mit 3:7, 16:6; 2 Nya 19:7; Kut 20:20; Zab 34:11, 14; Ayu 28:28; Mit 8:13).
     – Ina maana gani “kumtukuza Mungu?” Kumtukuza [Mungu] ni kumpa Mungu utukufu. Humaanisha kuakisi tabia yake ya haki katika maisha yako na matendo (Kut 33:18-23, 34:5-8; Mdo 10:35; 1 Kor 15:33-34; Zab 29:1-2, 86:7-13).
     – Ina maana gani tunaposema “saa ya hukumu yake imekuja?” Hii ina maana kwamba siku ya hukumu ya Mungu ilikuwa imefikia kuanzia Octoba 22, 1844 (“Evangelism,” ukr. 223; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 125; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 692). Wale waliochagua kumtumikia Mungu na wameendelea kuwa waaminifu kwake wangehesabiwa kwamba wanastahili uzima wa milele (“The Great Controversy,” ukr. 480; “Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 384), lakini wale wanaochagua kumkataa Mungu na njia zake alizoweka za ukombozi, na kuendelea katika dhambi, wangehukumiwa kama wasiostahili uzima wa milele (1 Pet 4:17; Rum 2:5-9; “The Great Controversy,” ukr. 482-486; “Early Writings,” ukr. 280). Dhambi zetu zote zinaandikwa katika vitabu vya kumbukumbu vya mbinguni kwa ajili ya hukumu (Dan 7:9-11; “The Great Controversy,” ukr. 487; “Christ’s Object Lessons,” ukr. 310), na inaanza kwanza na waliokufa, na hatimaye walio hai (“The Great Controversy,” ukr. 436; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 125). Hukumu haituweki huru toka dhambini, lakini inatuamsha kuona kwamba tuna muda mfupi, na kwamba lazima tuokolewe kupitia kwa Yesu kutoka katika nyumba ya gereza la dhambi kabla hatujahukumiwa mmoja mmoja na kuweza kusimama katika hukumu (“The Great Controversy,” ukr. 436), vinginevyo tutakumbana na mauti ya milele (Ufu 20:11-15).
     – Ina maana gani “Kumsujudia yeye?” Kumsujudia Mungu humaanisha kwamba tunamheshimu, kumtumikia na kumtii yeye pekee (Zab 96:9, 29:2, 5:7; 1 Nya 16:29; Mt 4:10; Yoh 4:23-24); kwamba utii wetu wa mambo ya kiroho ni kwa Mungu pekee na si mwanadamu yeyote au Kanisa au serikali au taifa au mamlaka (Mdo 5:29; Gal 1:10; Zab 118:6, 8-9).
     Huu ni sehemu ya ukweli ulio katika Ujumbe wa Malaika wa Kwanza ambao kwa huo Kanisa la SDA liliinuliwa na kusimikwa juu yake. Je, ukweli huu bado unafuatwa na Kanisa la SDA? Je, ukweli huu ni ujumbe pekee unaowekwa mbele ya watu, au Kanisa la SDA limebadilisha ukweli huu wa thamani wa Malaika wa Kwanza na kuwa ujumbe mchafu?
     Je, nini ambacho Kanisa la SDA linafundisha juu ya huu ukweli unaopatikana katika Ujumbe wa Malaika wa Kwanza?

     Kanisa la SDA linaamini nini juu ya Injili ya Milele ikiwa ni uhuru kutoka dhambi za nyuma kutokana na kupatanishwa, na kuepuka na kutenda dhambi kwa njia ya kuunganika na uungu katika kutumia nguvu ya matakwa yetu, kuweka jitihada zetu ili kushinda dhambi?
     “...‘injili ya milele’...ni wokovu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo bila kazi za matendo ya haki kwa upande wetu.” “Marked!”, ukr. 39, na Bob Spangler, Review and Herald Publishing Association, 1981.

     “Wokovu ni kwa neema tu kupitia imani. Hakuna zaidi.” “Signs of the Times,” Novemba, 1986, ukr. 19.

     “Muujiza wa neema…Chimbuko letu endelevu na pekee la wokovu.” “Adventist Review,” Aprili 21, 1983, ukr. 15.

     “Kwa pamoja mume wangu na mimi tulikuwa tumefanya uamuzi, baada ya kuhudhuria mfululizo wa mikutano ya makambi ya usiku iliyodhaminiwa na Kanisa la Waadventista, kuingia katika mahusiano ya agano na Yesu….Nilipumzika sasa katika imani yangu mpya, kukaa kitako, na kuacha Mungu afanye yaliyobaki.” “Adventist Review,” Juni 10, 1982, ukr. 10.
(Kauli zingine zinazofuata mkondo kama huo, angalia: “Adventist Review,” Oktoba 27, 1983, ukr. 5,  Oktoba 24, 1985, ukr. 5,  Juni 2, 1988, ukr. 10.)

     Je, nini kuhusu umuhimu wa kushinda dhambi kwa kuunganisha ubinadamu na uungu katika kutumia nguvu za matakwa yetu kwa kuweka juhudi na kupigana dhidi ya dhambi?
     “Injili si kufanya kitu chochote ili kuwa bora wenyewe. Si kujirekebisha wenyewe, kwa kutumia nguvu ya matakwa yetu kuacha tabia mbaya…hii siyo injili….Ni habari njema: si kwamba tutende lolote kwa ajili ya Mungu…ni wokovu kwa imani…‘Yote ni neema.’” “Voice of Prophecy News,” Februari, 1976, ukr. 6, H.M.S. Richards, Sr.

     “‘Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote’ (1 Yoh 1:9). Huku ndiko kuishinda dhambi...” “Cornerstone Connections Youth Quarterly,” 2nd Quarter, 1994, ukr. 62, Review and Herald Publishing Association.


     Fundisho hili la “yote ni ya neema,” “hakuna chochote” – au kwamba Kristo amefanya yote kwa ajili yetu kwa hiyo hakuna umuhimu wa kutunza amri za Mungu kwa ukamilifu; kwamba tunaokolewa “kwa imani pekee,” hebu “mwachie Mungu afanye yaliyobaki,” na kwamba Yesu atatii kwa ajili yetu na kutupatia yote yapasayo kwa ajili ya wokovu kama “karama” – ni fundisho lile lile ambalo Wanikolai walifundisha (Ufu 2:6, 15; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 957), ambalo Bwana huchukia!

     Bado fundisho hili la uongo linafundishwa wazi wazi bila aibu na kwa nguvu na washiriki wa Kiadventista.
     “Je, utii wetu kwa mapenzi ya Mungu (kama wengine wadaivyo) umejengwa kwa sehemu na juhudi zetu na sehemu ya juhudi za Mungu? Hasha! Hivyo sivyo ilivyo!”  “Marked,” Ukr. 129.

     “Kwa hiyo kama nikijikuta nashindwa kutii kikamilifu kama Yesu alivyofanya, sihitaji kutahayarishwa” “Obedience of Faith,” ukr. 43, na Morris L. Venden, Review and Herald Publishing Association, 1983.

     “Utii ni kwa imani, kujumlisha au kutoa bure. Utii ni kwa imani tu….Utii lazima uje kwa imani pekee…” Faith That Works,” ukr. 159, 161, na Morris L. Venden, Review and Herald Publishing Association, 1980.

     “Ni habari njema kujifunza kwamba utii ni kwa imani pekee, kadiri ambavyo msamaha ni kwa imani pekee.” “To Know God,” ukr. 96, na Morris L. Venden, Review and Herald Publishing Association, 1983.

     “Msamaha ni zawadi, wokovu ni zawadi, na utii ni zawadi…Yeye [Kristo] anataka kutupatia ushindi na kushinda kama zawadi.” “Ibid,” ukr. 101, 112.

     “Yote tunayoweza kufanya ni kuyakubali [utii, ushindi, na kushinda] kama zawadi”“Good News and Bad News about the Judgment,” ukr. 47, na Morris L. Venden, Pacific Press Publishing Association, 1982.

     “…kwa maisha yake makamilifu…yakikamilisha kwa dhati matakwa ya sheria kwa ajili ya mwanadamu.” “Marked,” ukr. 89.
     “Yeye [Kristo] hutupatia pumziko…kutoka katika jitihada zetu za kushinda dhambi na Shetani, na kuacha kupigana vita ambavyo Yesu ameahidi kutupigania….Kumbuka kwamba zawadi ni zawadi.” “Adventist Review,” Desemba 24, 1981, ukr. 5.

     Kama unavyoona, kuna tofauti ndogo kati ya injili ambayo Kanisa la SDA linafundisha sasa na injili ambayo Makanisa mengine ya Babeli yanafundisha!
     Ukweli ni kwamba Kanisa la SDA linakiri hili:
     “Kama Waadventista tunaamini katika kufundisha injili, sawa tu na Makanisa mengine yanayotuzunguka….Wote tunaokolewa kwa neema, si kwa kile tunachokifanya….
     “Kanisa la Waadventista Wasabato ni la pekee si katika kuhubiri injili, lakini katika mazingira ambayo injili hiyo inahubiriwa.” “Adventist Review,” Septemba 13, 1984, ukr. 7.

     Nini Kanisa la SDA linaamini juu ya Habari Njema ikiwa pekee juu ya Yesu Kristo?
     “…habari njema juu ya Kanisa la Waadventista Wasabato…” “Pacific Union Recorder,” Septemba 18, 1989, ukr. 12.

     Hivyo, injili si kuwaleta watu kwa Yesu Kristo, bali ni kuwaleta watu katika Kanisa la SDA! Agizo Kuu la injili la Yesu linahafifishwa kuwa “Ukuaji wa Kanisa” – kuleta washiriki, badala ya kufundisha ukweli na kuwaleta watu kwa Yesu.
     “[Mathayo 28:19-20 imenukuliwa]. Kanisa lina shughuli moja: Bwana aliyeteswa na kufufuka alituamuru kuwafanya wanafunzi wa kiume na kike kila mahali, na, baada ya kuwafanya hawa watu wanafunzi waaminifu, kuwafundisha kuwa wafanya wanafunzi.” “Adventist Review,” Aprili 7, 1988, ukr. 23.

     Je, Kanisa la SDA linaamini nini juu ya Kristo kuchukua asili ya Adamu baada ya kuanguka – au kuchukua asili ya kuanguka ya dhambi juu yake, na siyo kuwa na asili nyingine tofauti na ya mwanadamu?
     “[Yesu] Alichukua Hali Ya Asili Ya Kutokuwa Na Dhambi Ya Adamu Kabla Ya Kuanguka” “Movement of Destiny,” ukr. 497, na LeRoy Edwin Froom, Review and Herald Publishing Association, 1971.

     “...Yesu alikuwa na asili yote, kamili, isiyo na dhambi ya Adamu kabla hajaanguka.”“Salvation By Faith and Your Will,” ukr. 93, na Morris L. Venden, Southern Publishing Association, 1978.

     “...Waadventista waliamini kwamba asili ya kiroho ya Kristo iliakisi ile ya Adamu kabla ya kuanguka.” “Angry Saints,” ukr. 321, na George R. Knight, Review and Herald Publishing Association, 1989.
(Kauli nyingine zinazolandana na hili angalia: “Adventist Review,” Februari 1, 1990, ukr. 19-21.)

     Ikiwa Yesu hakuwa na asili ya kuanguka ya mwanadamu juu yake, basi ingekuwa rahisi kwake kushinda; na hivyo angezaliwa tofauti kuliko wewe na mimi katika jambo hili. Wanadamu walioanguka wasingestahimili kusimama dhidi ya dhambi kama hii ingekuwa kweli.
     Lakini Kanisa linafundisha nini?
     “Mwanadamu anatenda dhambi kwa sababu ni mdhambi. Si mdhambi kwa sababu anatenda dhambi….Hupaswi kufanya dhambi ili kuwa mdhambi; yote unayotakiwa kuyafanya ni kuzaliwa mwenyewe!...Yesu ndiye pekee aliyezaliwa akiwa na haki.” “To Know God,” ukr. 22-23.

     “Pasipo shaka Yesu alizaliwa tofauti. Alikuwa na asili ya kutotenda dhambi, kama ile aliyokuwa nayo Adamu kabla ya kuanguka kwake.…Kwa hiyo ilikuwa ni asili yake Yesu kuwa mwema. Nilizaliwa na asili ya dhambi, na ni asili yangu mimi kuwa mbaya.” “Salvation By Faith,” ukr. 86.
(Kkauli nyingine inayoendana nah ii angalia: “Adventist Review,” Juni 28, 1990, ukr. 8.)

     Ni habari gani juu ya Yesu kutotumia nguvu za uungu alipokuwa hapa duniani?
     “Kukubali, labda upande wa umilele usioelezeka, kuwa mbadala kwake [Kristo] kulilazimu [kutumia] uungu wake…[mwisho wa makala katika sehemu ya rejea za nukuu]…Kristo anachorwa…akiwa anatumia sifa zake za uungu.…Angeweza kutumia nguvu zake…” “Adventist Review,” Februari 1, 1990, ukr. 21-22.

     Nini habari ya Yesu kuwa na nguvu za pekee kuliko mwanadamu aliyeanguka?
     “Wakati Yesu alipochukua sifa za mwanadamu aliyeanguka, kuna moja ambayo hakuichukua – asili ya dhambi ya mwanadamu. Alikuwa na asili ya kiroho tangu kuzaliwa…Yesu hakuwa na tamaa ya kutenda dhambi. Waweza kusema hilo juu yako mwenyewe?...
     “Yote hii inatuongoza sisi katika swali la vitendo: Je, Yesu alikuwa na aina yoyote ya faida zaidi yetu? Ndiyo, alikuwa na kitu cha ziada zaidi yetu.” “Ministry,” May, 1982, ukr. 19.

     Ikiwa kweli Yesu alizaliwa na asili ya kutotenda dhambi ya mwanadamu, akatumia nguvu zake za uungu, na alikuwa na fursa ya ziada kuliko mwanadamu aliyeanguka, basi angekuwa mfano kamili na kielelezo au Mwokozi kutoka katika dhambi zetu. Asingejua kamwe kile kilichokuwa kinatusumbua ndani pale tunapojaribiwa, wala jinsi ya kusaidia na kutupa nguvu kushinda dhambi tukiwa na asili ya kuanguka juu yetu; angejua tu jinsi ya kuwafariji na kuwasaidia wale ambao wana asili ya kutoanguka! Hivyo Kristo kama Mwokozi wetu kutoka dhambini angepokonywa kwa hakika kutoka kwetu, na tusingeshinda dhambi! Hatimaye tungepotea kama hii ni kweli.

     Lakini, nini kinachofundishwa na Kanisa la SDA?
     “Kwa sababu ubinadamu [asili] haukuwa na dhambi, Yesu asingeweza kupitia misukumo…ya ndani ya wanadamu wadhambi.” “Adventist Review,” Februari 1, 1990, ukr. 21.

     Nini ambacho Kanisa la SDA huamini juu ya ufafanuzi wa dhambi ukiwa ni uasi wa amri za Mungu?
     “Dhambi…ni maisha yoyote ambayo yako mbali na Mungu.” “To Know God,” ukr. 22.

     “Unaona, Kwa Baba dhambi ni uhusiano uliovunjika, na si tabia mbaya inayoeleweka….Kwa hiyo kwa kielelezo cha urafiki wa dhambi kuliko kielelezo cha tabia, unajibu swali ‘Je, ni dhambi ku?”’ “Guide,” August 10, 1991, ukr. 23, Review and Herald Publishing Association.

     “Watu wengi hudhani kwamba dhambi ni kufanya mabaya, kuvunja sheria, na mengineyo….Dhambi humaanisha kutengwa kutoka kwa Mungu.” “Cornerstone Connections Youth Quarterly,” ukr. 56-57.
     “Dhambi ni kile tu ambacho unataka kukifanya lakini mamlaka fulani iliyo dhahiri haikuruhusu kuifurahia…” “Signs of the Times,” November, 1992, ukr. 5.
(Kauli nyingine sawa sawa nah hii iko katika “Insight,” Machi 12, 1994, ukr. 15.)

     Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya Upatanisho au kuhesabiwa haki? Je, ni “ikiwa uliokolewa basi utaendelea kuokolewa?”
     “…kuna kupatanishwa [kuokolewa] kwa aina moja, na humfuata mwumini kutokea wakati wa kuingia katika imani…na safari yote mpaka hukumu ya mwisho.” “Adventist Review,” August 11, 1983, ukr. 4.

     “Kupatanishwa [kuhesabiwa haki] humaliza mambo yetu yote wakati huu, lakini inatumika pia kwa wakati wa baadaye kama mwamvuli unaofunika tokea wakati tunapomkubali Kristo mpaka tutakapokutana na Bwana.” “Marked,” ukr. 125.

     Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya Utakaso, na Ukombozi? Je, kuunganisha imani na matendo ni muhimu kwa utakaso na wokovu?
     “Wokovu bado unatolewa kwa watu kwa misingi tu ya imani yao katika Yesu Kristo, si kwa sababu ya kutunza sheria ya Mungu kwa uaminifu au sehemu za sheria za muhimu.” “Adventist Review,” Aprili 12, 1984, ukr. 9.

     “Watu wengi hukubali wazo kwamba kupatanishwa ni kwa imani pekee, lakini wanajikuta katika mazingira magumu kulipa kisogo wazo kwamba kuna kitu ambacho tunaweza kukifanya wenyewe katika tendo zima la utakaso. Wengine hudhani wazo hili kuwa hatari kuliacha kwamba utaratibu wa kuishi maisha ya Kikristo ni kwa imani ukijumlisha na kazi za matendo….Ikiwa tutaweka juhudi zetu na matakwa ya maisha yetu kukamilisha kile ambacho si rahisi kwetu kikifanya [kutunza amri za Mungu na kushinda dhambi], basi tutaishia kushindwa.” “Faith That Works,” ukr. 188.

     “Je, tunaweza…kupokea nguvu [neema ya Mungu] kushinda hali yetu ya kutenda dhambi? Jibu ni hapana. Utakaso ni zawadi tu ya Mungu kama ilivyo kuhesabiwa haki.” “Ministry,” Januari, 1982, ukr. 6.

      “Yote matatu (upatanisho, utakaso, na kutukuzwa] yameunganishwa katika wokovu, na vyote huja kama zawadi kutoka kwa Yesu…” “Faith That Works,” ukr. 191.

     “Yeye [Kristo] alimaliza yote, kwa wote, utakaso wetu na ukombozi. Hakuna anayeweza kuongeza kwa lile alilolifanya” “Seventh-day Adventists Believe...A Biblical Exposition of 27 Fundamental Doctrines,” ukr. 128, Review and Herald Publishing Association, 1988.
(Kauli zingine zenye dhana hiyo hiyo angalia “Adventist Review,” Julai 28, 1983, ukr. 8; Machi 22, 1984, ukr. 4.)

Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya Yesu kutuokoa kutoka katika dhambi zetu, si katika dhambi zetu?
     “Mungu hututangazia kupatanishwa, au kuwa na haki, kabla tabia zetu hazijabadilishwa. Mungu hutukubali kama wana na binti zake hata kabla hatujatenda kama wana na binti.” Marked,” ukr. 105.

     “…Mungu alichukua hatua ya kuwasamehe na kuwakubali katika dhambi zao…” “Adventist Review,” Januari 7, 1988, ukr. 14.

     Je, Kanisa la SDA linaamini nini juu ya kumcha Mungu na kutunza amri zake na kutoka katika dhambi?
     “…hakuna tunachoweza kukifanya kamwe ambacho kinaweza kutupatia ukubali kwa Mungu.” “Questions On Doctrines,” ukr. 108, Review and Herald Publishing Association, 1957.

     “Jitihada za mtu kutii sheria ya Mungu, hata kama ni za dhati, haziwezi kamwe kuwa uwanja wa wokovu. Tunaokolewa kwa njia ya…imani pekee. Kafara ya Bwana wetu Kalvari ndiyo pekee tumaini la mwanadamu.” “Ibid,” ukr. 190.

     “Ni makosa kwa mtu kujaribu kuishi maisha ya Kikristo. Hatujatakiwa kufanya hivyo.” “Salvation By Faith,” ukr. 40.

     Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya kumpa Mungu utukufu tu kwa kuakisi tabia yake ya haki katika maisha yako?
     “Unampa Mungu utukufu kwa kuwa na tahadhali na vitu vionyeshavyo kuwa ‘Yuko hai na upendo’ usioeleweka, wa juu juu wa mtoto wa mbwa, muujiza wa nguvu za vitu vigumu ambao ni wa nyuki mkubwa, utamu mgumu wa tikiti maji lililokomaa, kumbatio lenye unyevunyevu la mtoto wa wakati wa kitandani, mapigo ya maisha yaliyopangiliwa katika shingo yako.” ”Signs of the Times,” Machi, 1993, ukr. 15.

     Nini Kanisa la SDA linaamini juu ya kumsujudia Mungu tu na Yeye pekee?
     “Swali la msingi si jinsi ya kuabudu, lakini nani wa kuabudu…Kuabudu humaanisha kwamba injili ya uzima inaenea kwa kila taifa, kabila, lugha, na jamaa. Kuabudu humaanisha kuelekeza kila kitu kwa Mungu ambaye anapenda nchi tulimozaliwa hata zaidi kuliko sisi tulivyo....Kuabudu humaanisha kupokea tumaini la Yerusalemu Mpya wakati tukiishi na Babeli kutuzunguka.” “Adventist Review,” Desemba 31, 1992, ukr. 10.

     Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya kutoa maisha yetu kiroho kwa Mungu tu?
     “Baraza la Waadventista Wasabato, basi, ni Kanisa la Waadventista Wasabato….Ukamilifu wa Kanisa la Masalio kama Dhehebu la Kikristo, katika jumuiya ya ulimwengu uliounganishwa ambamo Waadventista Wasabato wanawiwa utii.” “Equal Employment Opportunity Commission [US Government] vs Pacific Press Publishing Association [SDA Church],” Civ #74-2025 CBR, ukr. 17 (trial proceedings from 1974-1975).

     Nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya saa ya hukumu ya Mungu imekuja dhidi ya dhambi; kwamba lazima tufunguliwe kutoka katika kifungo cha nyumba ya dhambi kabla hatujahukumiwa mmoja mmoja; kwamba dhambi zetu zote zikiwa zimeandikwa katika vitabu vya kumbukumbu vya mbinguni, na kama tukikutwa na dhambi ambayo haijaachwa, basi tutahukumiwa kama tusiofaa kupata uzima wa milele na hivyo tutalaaniwa katika dhambi kwa ajili ya maangamivu?
     “Shetani amefanikiwa wakati huu tena kwa kuwafanya watu wa dini kuamini kwamba wakati wanapoanguka, wanahesabiwa laana.” “Faith That Works,” ukr. 192.

     “…[Waadventista] huogopa kuvunja sheria na kuhesabiwa kama wasiofaa katika hukumu. Huo siyo Ukristo.” “Angry Saints,” ukr. 143.

     “…je, tunapaswa kuogopa hukumu ya Mungu? Je, habari kwamba siku ya hukumu ya Mungu imekuja (angalia Ufu 14:6, 7) ni habari mbaya au njema?...
     “Kwa wale wenzetu ambao wamekuwa wanaishi maisha katika kifungo cha nyumba ya Shetani, wakiwa wamepigwa na kujeruhiwa na adui wakati wakiishi katika ulimwengu huu wa dhambi, ni habari njema kwamba hukumu inakuja haraka na kwamba haki ya Mungu itapatiliza dhambi zilizotendwa. Ina maana kwamba hifadhi yetu sasa imekwisha. Saa ya kutolewa kwetu imekaribia.” “Signs of the Times,” Novemba, 1986, ukr. 13.

     Nini juu ya dhambi zetu kuwekwa katika kumbukumbu katika vitabu vya mbinguni kwa ajili ya hukumu ya upelelezi?
     “...Mungu hatunzi kumbukumbu ya dhambi zetu kule [juu mbinguni]…” “Adventist Review,” Septemba 8, 1988, ukr. 10.

     Kanisa la SDA sasa linafundisha kwamba hukumu inayokuja itatuondoa katika gereza la nyumba ya dhambi, lakini si kutuhukumu kwa kuendelea kufanya dhambi.  Hivyo, watu wanaamini kwamba hakuna haja kuachana wenyewe na dhambi za binafsi kabla ya kuhukumiwa, kwa sababu hukumu ingeondoa dhambi zao binafsi kwa ajili yao!  Watu wanaambiwa pia kwamba hakuna kumbukumbu ya dhambi zetu katika vitabu vya mbinguni. Hivyo watu wanaamini kwamba dhambi ambazo hazijaachwa haziwezi kuwa kigezo cha kutuhukumu kama tusiostahili kuingia mbinguni na kupokea uzima wa milele!
     Basi ni kigezo kipi ambacho Kanisa la SDA linafundisha?
     “…mandhari ya hukumu…hufanya dhahiri kwamba kigezo cha kutathmini kustahili katika ufalme ni jinsi tunavyohusiana na wale walio wagumu sana kuhusiana nao: wanaougua na waliosetwa.” “Adventist Review,” Januari 7, 1988, ukr. 14 (msisitizo wa awali).

     Kwa hiyo bila ya kutunza kumbukumbu ya dhambi zetu, na hukumu ikituweka huru kutoka katika dhambi zetu badala ya kutuhukumu katika hizo, ni namna gani mtu aweza kuhukumiwa, au kuangamia, au kupotea? Na kama hakuna hata mmoja anayepotea, basi kila mmoja ataokolewa!  Je, Kanisa la SDA linaamini kwamba hakuna atakayeangamia au kupotea?
     “Neno potea katika Agano Jipya halimaanishi kwamba mtu anahukumiwa kwenda motoni au kupotea.” “Adventist Review,” Aprili 1, 1993, ukr. 21. (ANGALIA: Strong’s Exhaustive Concordance of the Bible hutafsiri “kupotea” (# 622) kumaanisha “kuharibu, kufa, kupotea, toweka, angamia.”)

     Kwa hiyo Kanisa la SDA sasa linafundisha kwamba mtu anaangamia; hivyo nani atapotea?

     Kanisa la SDA limebadilisha Injili ya Milele, kuwa fundisho la wanikolai ambao Mungu anawachukia! Wanafundisha kwamba Kristo alikuwa na nafasi ya pekee kuliko mwanadamu katika uwezekano wa kushinda dhambi, hivyo kwa hakika wamemwiba Kristo kutoka kwa watu kama Mwokozi wa kila mtu anayetuokoa toka dhambini, kwenda katika Mwokozi anayetuokoa katika dhambi. Wamebadilisha “mcheni Mungu” na kutunza amri zake za haki, katika kumcha Shetani na kutunza amri zake! Wamebadilisha “kumpa Mungu utukufu” kwa kuakisi tabia yake ya haki, kwenda katika kumpa Shetani utukufu kwa kuakisi tabia yake isiyokuwa ya haki! Wamebadilisha “msujudiaeni Mungu” peke yake na mpatie mambo yako yote kiroho, katika abudu mambo mengine na toa utii wako wote kiroho kwa Kanisa la SDA na uongozi wake! Na wamebadilisha hukumu ya Mungu dhidi ya dhambi, kwenda katika kutuokoa kutoka katika dhambi za binafsi! Hivyo, hakuna aliye hatarini kuangamia katika hali ya kupotea, lakini wataokolewa katika dhambi zao.
Tunaweza kuona dhahiri kwamba Kanisa la SDA limebadilisha ukweli wa Ujumbe  Malaika wa Kwanza katika ujumbe wa uongo, ufungwa na uchafu. Kwa hiyo Kanisa la SDA limekataa ukweli wa Ujumbe wa Malaika wa Kwanza, na limeweka mahali pake, na kuingiza, ujumbe wa roho mchafu wa kwanza!

     Je, nini habari ya Ujumbe wa Malaika wa Pili?


UJUMBE WA MALAIKA WA PILI

     “Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka, Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya gadhabu ya uasherati wake.” Ufu 14:8.

     Babeli iliyoanguka huwakilisha kuanguka kwa Makanisa ya Kiprotestanti mwaka 1844 kwa sababu yalikataa nuru na ukweli wa Ujumbe wa Malaika wa Kwanza kutoka mbinguni (“Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 13; “Early Writings,” ukr. 274; “The Great Controversy,” 381-383).
     Kanisa la Kikatoliki la Kirumi lilikuwa tayari limeshakuwa Babeli karne nyingi kabla ya 1844, na Mungu alikuwa amechagua Makanisa ya Kiprotestanti kudhihirisha ukweli wake kwa ulimwengu. Lakini yalikuwa, kama jamii iliyounganika, yamechagua kuondoka upande wa Kristo – mume wake, na kujiunga yenyewe na ulimwengu. Mungu kwa rehema zake alituma Ujumbe wa Malaika wa Kwanza kuvunja upendo wa ukahaba na ulimwengu, na kuyarejesha tena upande wake kama mwanamwali mwaminifu tena. Lakini yalikataa, na hivyo yakawa Babeli iliyoanguka (“Spirit of Prophecy,” vit 4, ukr. 230-240). Na mvinyo ya Babeli ni mafundisho ya uongo ya Kanisa Katoliki la Kirumi yaliyo msingi wake – ikiwa kutunza Jumapili na roho kutokufa (“Evangelism,” ukr. 365; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 317: “The Great Controversy,” ukr. 536; “Selected Messages,” kitabu cha 2, ukr. 118; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 979).
     Je, Kanisa la SDA bado linafundisha kwamba Babeli huwakilisha Roma na Uprotestanti ulioasi? Nini Kanisa la SDA huamini kwamba Babeli inawakilisha leo?
Kanisa la SDA linaamini kwamba Babeli ni:
     – “mji mwovu” wa kisasa (“Signs of the Times,” Juni, 1992, ukr. 29).
     – “uovu wa mji wangu” (“Adventist Review,” Desemba 31, 1992, ukr. 9).
     – “mivuto ya uovu” (“Signs of the Times,” Juni, 1992, ukr. 29).
     – “adui mkuu wa Kristo na Kanisa lake” (“Adventist Review,” Julai 13, 1989, ukr. 11).
     – “bado inawakilisha mwelekeo wa mawazo” (“Signs of the Times,” May, 1992, ukr. 13).
     – “kumwabudu yeyote badala ya Mungu pekee” (“Adventist Review,” Oktoba 15, 1992, ukr. 11).
     – “kukubaliana katika mambo ya kiroho” (“Signs of the Times,” Special Issue, 1985, ukr. 8).
     – “kujaribu kupata wokovu kwa njia ya matendo ya sheria ya mtu mwenyewe” (“Adventist Review,” Desemba 31, 1992, ukr. 9; angalia pia “Marked,” ukr. 150).
     – “…dhana kwamba naweza kujiokoa mwenyewe au kwamba naweza ‘kutenda hilo mwenyewe’ kwa njia ya kuishi maisha ya Kikristo au kwenda mbinguni” (“The Return of Elijah,” ukr. 61, na Morris L. Venden, Pacific Press Publishing Association, 1982).
     – “... jaribio lisilo na faida la kujenga maisha ya mtu katika kujaribu kwa jitihada au kanuni ya fanya-kama upendavyo…wote kwa pamoja mataifa na pia mtu binafsi…” (“Adventist Review,” Septemba 7, 1989, ukr. 26).
     – “ubaguzi umeanguka, hali kadhalika kutotendewa haki watoto, vikosi vya mauaji, upweke, ufa, mateso, utengano, kifo” (“Adventist Review,” Desemba 31, 1992, ukr. 9).
     – “Kuanguka kwa Umoja wa Urusi” (“Signs of the Times,” May, 1992, ukr. 12-13).

     Na wito wa kutoka Babeli sasa:
     – “kukimbia uovu” (“Adventist Review,” Februari 16, 1984, ukr. 7).
     – “kutoka katika madanganyifu” (“Signs of the Times,” Machi, 1990, ukr. 28; angalia pia “Marked,” ukr. 83).
     – “kuweka mbali asili yetu ya kujiona na majivuno na kumpa Mungu matashi yetu” (“Marked,” ukr. 84).

     Je, nini habari ya mvinyo ya Babeli yakiwa ndiyo mafundisho yake ambayo (Kanisa la Kikatoliki la Kirumi) limejijenga – yaani utunzaji wa Jumapili na roho kutokufa ambavyo vimetokana na msingi mkuu wa Babeli – Utatu Mtakatifu?
     “Itikadi ya maendeleo ya ulimwengu unaoendelezwa – kwamba mwanadamu ana majibu kwa shida zinazokikabili kizazi hiki; kwamba kama angepewa muda mdogo zaidi, angeweza, bila msaada wa ki-Mungu, kuleta ulimwengu mzuri – ndiyo mvinyo ya kulevya ambayo Babeli imeuuzia ulimwengu mzima.” “Adventist Review,” Septemba 7, 1989, ukr. 26).


     Kulingana na Kanisa la SDA, Babeli iliyoanguka ni chochote lakini si Kanisa lililoanguka kwa kunajisiwa! Watu hawahitajiki tena kujitenga wenyewe kutoka katika Kanisa Katoliki la Kirumi, au Makanisa ya Kiprotestanti, au Kanisa lolote lililoasi kwa unajisi; lakini kutoka katika miji iliyojaa uovu, mivuto ya uovu, adui mkubwa, madanganyifu, dhana fulani potofu na mitizamo, kufanya urafiki na dhambi, kufanya kazi kwa ajili ya wokovu wetu, ubaguzi wa rangi, kutowatendea haki watoto, vikosi vya mauaji, upweke, ufa, mateso, kutengana, vifo, na Jumuiya ya Kirusi. Mvinyo yoyote ya Babeli si kutunza Jumapili, lakini jitihada za mwanadamu kufanya ulimwengu huu uwe mzuri zaidi!
     Tunaweza kuona dhahiri kwamba Kanisa la SDA limebadilisha ukweli wa Ujumbe wa Malaika wa Pili kwenda katika vitu visivyoeleweka zaidi, madanganyifu, na limewaweka watu kwenye kifungo cha Babeli Halisi. Kwa hiyo Kanisa la SDA limekataa ukweli wa Ujumbe wa Malaika wa Pili, na limeweka badala yake, na kuingiza, ujumbe wa roho ya pili ya uchafu!

     Je, nini habari ya Ujumbe wa Malaika wa Tatu?


UJUMBE WA MALAIKA WATATU

     “Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kupokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo. Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, na hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujudiao huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake….
     “Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake. Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza; kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya gadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake. Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.” Ufu 14:9-11; 18:1-5.

     Ujumbe wa Malaika wa Tatu kwa dhahiri unarudia ujumbe wa malaika wa Kwanza na wa Pili. Hata hivyo hauishii hapa tu, lakini unafunua maeneo kadhaa ya ukweli.
     Ukweli kama:
     – Siku ya saba au Jumamosi ikiwa ndiyo pekee siku ya Bwana kama Sabato (Mwa 2:2-3; Ufu 1:10; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 128), kwamba ni alama au muhuri wa Mungu (Eze 20:12, 20), na hakuna ukweli wa kibiblia kuunga mkono mabadiliko kuelekea Jumapili kama siku ya Bwana (Kut 20:8-11; Ebr 4:3-11; Eze 20:12-20; 1 Nya 17:27), hivyo tunapaswa kuitunza Sabato ikiwa tunahitaji kuingia mbinguni (“Early Writings,” ukr. 37; “The Desire of Ages,” ukr. 206; “Testimonies for the Church,” vit 8, ukr. 196-198; “The Great Controversy,” ukr. 455; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 349; “Prophets and Kings,” ukr. 182; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 949; “Testimonies for the Church,” vit 3, ukr. 392; “Evangelism,” ukr. 290; “Testimonies for the Church,” vit 1, ukr. 532, vit 2, ukr. 705; “Life Sketches,” ukr. 117-118).
     – Uhuru wa Dini, ukiwa ni haki iliyotolewa na Mungu kujifunza, kusimamia, na kutangaza ukweli wake tu, na kuweka wazi makosa (“The Great Controversy,” ukr. 563-566; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 714-716; “Testimonies to Ministers and Gospel Workers,” ukr. 200-203; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 402-403).
     – Mnyama akiwa Ukatoliki wa Kirumi (Ufu 13:1-8; Dan 7:8-14, 20-21, 24-27, 8:9-14, 23-25; “The Great Controversy,” ukr. 438-450; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 972), pamoja na msingi wa Kanisa hili ukiwa ni Ekaristi – “makufuru” makubwa na “uzushi wa kutukana mbingu” (“Spirit of Prophecy,” vit 4, ukr. 63). Pia Papa na mfumo wa Kikatoliki kama Mpinga kristo (“The Great Controversy,” ukr. 142-143; “Testimonies to Ministers and Gospel Workers,” ukr. 37), na kazi yetu ni kufunua mambo yake na upapa (“Evangelism,” ukr. 233; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 196).
     – Mnyama aliye mfano wa Mwanakondoo, akiwa ni Marekani, ambaye anaipa uhai Sanamu ya Mnyama (Ufu 13:11-17; “The Great Controversy,” ukr. 440-445).
     – Sanamu ya Mnyama, ikiwa ni Makanisa ya Kiprotestanti ambayo yataungana katika mafundisho wanayokubaliana bila hitilafu [Utatu Mtakatifu uliozaa roho kutokufa, pumziko la Jumapili, n.k] ikiwa ni pamoja na Baraza la Umoja wa Makanisa – WCC (Ufu 13:15-18; “The Great Controversy,” ukr. 443-450; “Selected Messages,” kitabu cha 3, ukr. 385). Sanamu hii inafanywa baada ya Kanisa la SDA kuasi wakati Makanisa yanapoungana pamoja kwenye jukwaa la imani moja katika Kristo, na “kuihamasisha serikali kulazimisha makubaliano yao na mafundisho yao” (“Spirit of Prophecy,” vit 4, ukr. 277-278).
     – Alama ya Mnyama, ikitolewa kwa wote wanaoabudu Jumapili baada ya kuwa imefanywa sheria, wakati wakijua kwamba siyo Sabato ya Mungu (Ufu 13:16-17; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 976-980; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 17, vit 8, ukr. 159; “The Great Controversy,” ukr. 449-450, 578-579); hivyo hatupaswi kuyatii mamlaka ya kiserikali kulingana na sheria hii (“Selected Messages,” kitabu cha 2, ukr. 375, 380; “Testimonies for Ministers and Gospel Workers,” ukr. 473; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 910; “Testimonies for the Church,” vit 6, ukr. 193; “Fundamentals of Christian Education,” ukr. 287; “The Great Controversy,” ukr. 449).
     – Roho kutokufa (Ayu 4:17; 1 Tim 6:15-16; Ebr 9:27), kwamba kuna kaburi tu la kupumzika baada ya kifo (1 Kor 15:51; Mdo 13:36; Zab 88:10-12; Mhu 9:5-6). Na zawadi ya kutokufa pekee itakayotolewa kwa wenye haki Kristo ajapo mara ya pili (2 Tim 2:11-12; Ayu 19:26-27; Ufu 20:4-6; 1 The 4:16; 1 Kor 15:51-52; “The Great Controversy,” ukr. 549-551, 586-587; “Testimonies for the Church,” vit 1, ukr. 344; “Gospel Workers,” ukr. 119-120).
     – Hasira ya Mungu, yakiwa ni mapigo saba halisi ya mwisho (Ufu 16; “Early Writings,” ukr. 44, 64, 289-290; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 211, 634, vit 9, ukr. 234-235).
     – Hema Takatifu ya mbinguni (“The Great Controversy,” ukr. 324-329, 351-353, 398-400, 409-436; “Patriarchs and Prophets,” ukr. 351-358) ikiwa na vyumba viwili (Ebr 9 & 10) – patakatifu (Ufu 4:1-5; Ebr 9:2, 6, 12, 6:19; Law 16:15) na patakatifu mno (Ufu 11:19; Ebr 9:3-5, 7; Zab 28:2; 1 Fal 6:16, 8:6; 2 Nya 5:7; Kut 40:3).
     – Kazi ya Yesu ya upatanisho katika chumba kitakatifu mno, au chumba cha pili cha hema ya mbinguni, inayoendelea tangu Oktoba 22, 1844 mwisho wa siku 2300, na siyo mwisho mpaka atapomaliza kazi yake muda mfupi tu kabla ya kuja tena (“The Great Controversy,” ukr. 400, 419-422; “Early Writings,” ukr. 251-254; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 933; “Patriarchs and Prophets,” ukr. 355-358; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 472-473).
     – Kristo kama Kichwa au Mchungaji wa Kanisa lake (“SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1083; “Acts of the Apostles,” ukr. 360; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 93; “Testimonies for the Church,” vit 1, ukr. 78, vit 4, ukr. 393; “The Desire of Ages,” ukr. 288; “Sons and Daughters of God,” ukr. 303), pia Kuhani wetu mkuu, na Mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu (Ebr 7, 8 & 10; “SDA Bible Commentary,” vit 5, ukr. 1145,  vit 6, ukr. 1061, 1077-1078, 1116; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 243, 332).
     – Kanisa la kweli la Mungu, likiwa limejengwa juu ya Kristo na ukweli wake (“The Desire of Ages,” ukr. 413; “Acts of the Apostles,” ukr. 175-176, 595-596; “Testimonies for the Church,” vit 9, ukr. 147; “Prophets and Kings,” ukr 595-596), na alama za Kanisa la kweli zikiwa zimeorodheshwa katika Ufunuo 12:17 na 14:12; ambazo ni “kushika amri za Mungu,” na kuwa na “Ushuhuda wa Yesu Kristo” (“The Great Controversy,” 453-454) ambao ndiyo “roho ya unabii” (Ufu 19:10) au Maandiko ya Ellen G. White (“Testimonies to Ministers and Gospel Workers,” ukr. 114; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 27, 41; “Evangelism,” ukr. 257; “Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 13). Hivyo maandiko haya yana kusudi lake endelevu, na bado yanapaswa kufuatwa leo (“Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 48-50; “Life Sketches,” ukr. 198; “The Publishing Ministry,” ukr. 361; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 64, 654, 672-691, vit 3, ukr. 257, 260)!
     – Haki ya Kristo: zawadi hii ya pekee ambayo inategemeana na utii (“Sons and Daughters of God,” ukr. 189, 369; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 377; “Christ’s Object Lessons,” ukr. 223; “Prophets and Kings,” ukr. 591) inawekwa kwa imani kwa kila mdhambi anayetubu (“SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1071-1072; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 392, 397, 317, 363; “Sons and Daughters of God,” ukr. 240; “Testimonies for the Church,” vit 5, ukr. 469, vit 3, ukr. 371-372, vit 8, ukr. 208-209; “Gospel Workers,” ukr. 161; “My Life Today,” ukr. 311; “Thoughts from The Mount of Blessing,” ukr. 115-116: “Medical Ministry,” ukr. 115), na inatuwezesha kukubalika tena kwa Mungu (“Patriarchs and Prophets,” ukr. 353), na hatimaye kupokea neema yake (“Patriarchs and Prophets,” ukr. 431; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 351). Neema hii hutuwezesha kushinda dhambi, kukamilisha utakatifu katika kumcha Mungu kabla ya ujio wa pili wa Kristo (“Prophets and Kings,” ukr. 175; “Testimonies for the Church,” vit 4, ukr. 567, vit 3, ukr. 528, vit 5, ukr. 744; “Testimonies for the Ministers and Gospel Workers,” ukr. 92, 150; “The Desire of Ages,” ukr. 555-556; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 395; “Acts of the Apostles,” ukr. 531; “Sons and Daughters of God,” ukr. 315). Tunapaswa kutumia nguvu ya utashi wetu kuchukua hatua ya kwanza kwa utii kwa Mungu kabla neema haijaja kutusaidia kushinda (Yos 3:13, 15-17; “My Life Today,” ukr. 100) na haki ya Kristo inayotolewa kwetu kutusaidia (“SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 972, vit 6, ukr. 1096; “Evangelism,” ukr. 596; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 241; “Testimonies for the Ministers and Gospel Workers,” ukr. 92; “Messages to Young People,” ukr. 35; “The Desire of Ages,” ukr. 439). Sheria ya Mungu bado inamfunga Mkristo leo, na Kristo kuitunza hakutuweki huru kutokuitunza kamwe (“Testimonies for the Ministers and Gospel Workers,” ukr. 94, 131; “Sons and Daughters,” ukr. 240; “SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1073). Kukamilika si pale pale (“Sanctified Life,” ukr. 10, 92; “Messages to Young People,” ukr. 114; “Testimonies for the Church,” vit 3, ukr. 325, vit 8, ukr. 312-313, vit 1, ukr. 340, vit 2, ukr. 472; “Acts of the Apostles,” ukr. 560-561; “SDA Bible Commentary,” vit 7, ukr. 947; “Christ’s Object Lessons,” ukr. 65-66; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 317), lakini inaendelea katika maisha yetu yote wakati tukishindana na kusonga mbele katika njia nyembamba iliyonyooka kwenda mbinguni (“Acts of the Apostles,” ukr. 533, 560-561; “Testimonies for the Church,” vit 2, ukr. 170, 408-409, 479; “Messages to Young People,” ukr. 73, 144-145; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 28; “Fundamentals of Christian Education,” ukr. 218; “Christ’s Object Lessons,” ukr. 315; “SDA Bible Commentary,” vit 5, ukr. 1085; “Testimonies to Ministers and Gospel Workers,” ukr. 150). Hivyo, wakati tupo duniani, hakuna aliyeokolewa, au anayeweza kusema au kuhisi kwamba ameokolewa mpaka atakapofika mbinguni (“Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 314, vit 3, ukr. 354). Vazi la haki la Kristo haliwezi kufunika uovu wowote wala dhambi ambayo haijatubiwa. Hivyo, hakuna yeyote anayeweza kupata wokovu huku akiendelea katika dhambi (“Faith I Live By,” ukr. 113, “Christ’s Object Lessons,” ukr. 312; “Review & Herald,” vit 2, ukr. 232, “Signs of the Times,” vit 2, ukr. 307, vit 3, ukr. 363; “Selected Messages,” kitabu cha 1, ukr. 396; “Lift Him Up,” ukr. 150; “SDA Bible Commentary,” vit 6, ukr. 1072; “The Desire of Ages,” ukr. 555-556).


     Je, Kanisa la SDA bado linaamini na kufundisha ukweli huu wa Malaika wa Tatu, au wameubadilisha pia ukweli huu wa thamani katika upotofu?

     Je, namna gani siku ya Saba ikiwa tu siku ya Bwana ya ibada kama Sabato, kwamba ndiyo alama au muhuri wa Mungu, kwamba hakuna kitu chochote kinachounga mkono badiliko kwenda Jumapili kama siku ya Bwana, na kwamba tunapaswa kutunza Sabato ikiwa tunahitaji kuingia mbinguni?
     “Mungu anatufurahia tukienda kanisani siku zote mbili [Jumamosi na Jumapili]. Anatutaka tumwabudu Yeye katika siku zote mbili….Yeyote anayechukua siku nzima kutoka katika kila wiki kuitumia pamoja na Mungu atakuwa na nguvu zaidi za Mungu katika maisha yake, na Mungu anaweza kufanya mengi kupitia kwake.” “Signs of the Times,” Machi, 1990, ukr. 22-23.

     “…kirai ‘siku ya Bwana katika’ Ufunuo 1:10….Umakini zaidi unapaswa kuelekezwa katika uwezekano kwamba kirai kinaelezea juu ya sherehe ya ufufuo ya mwisho wa mwaka.” “The Sabbath in Scripture and History,” ukr. 127, Review and Herald Publishing Association, 1981.

     Siku ya “sherehe ya ufufuo wa mwisho wa mwaka” ni Jumapili ya Pasaka. Kwa hiyo Kanisa la SDA linafundisha kwamba “siku ya Bwana” au Sabato, si Jumamosi tu, lakini yaweza pia kuwa Jumapili! Kwa hakika hoja hii haisumbui hata kidogo kwa Kanisa la SDA, kwa sababu “Mungu anatufurahia sisi kwenda kanisani siku zote mbili.”
     Wakati uongozi wa Kanisa la kwanza la Kikristo ulipoamua kuungana na wapagani, Kanisa lilinajisiwa na mahali pake Kanisa Katoliki la Roma likazaliwa (angalia “Spirit of Prophecy,” vit 4, ukr. 42-46, 195, 396). Viongozi wake hatimaye walitupilia mbali Sabato ya kweli, na wakatumia hatua kuu mbili kuwaongoza washiriki wake waliokuwa wanatunza Sabato katika kuabudu siku ya Jumapili.
     “Katika karne za kwanza Sabato ya kweli ilikuwa imetunzwa na Wakristo wote. Walikuwa na wivu kwa ajili ya utukufu wa Mungu, na, hali wakiamini kwamba sheria yake haitanguki, walilinda kwa bidii utakatifu wa mausia yake. Lakini kwa udanganyifu wa hali ya juu, Shetani alifanya kazi kupitia mawakala wake kutimiza kusudi lake. Kwamba ili kuvuta mwelekeo wa watu kwenye Jumapili, ilifanywa sikukuu kuenzi ufufuo wa Kristo. Huduma za kidini ziliendeshwa siku hiyo…
     “ Hatua nyingine lazima ichukuliwe; Sabato ya uongo lazima iinuliwe katika usawa uleule kama ile ya kweli….Askofu wa Roma aliipa heshima Jumapili kwa kichwa cha siku ya Bwana.” “Spirit of Prophecy,” vit 4, ukr. 55.

     Hatua mbili zilikuwa: kuanza kuwa na ibada ya mapambazuko ya Jumapili ya Pasaka ili kuheshimu ufufuo wa Kristo, na kuanza kuita Jumapili siku ya Bwana.  Hatua hizi mbili zinaendelea ndani ya makanisa ya SDA kote duniani; huduma za mapambazuko ya Jumapili ya Pasaka ni kitu cha kawaida katika makanisa ya SDA. Pamoja na hayo, si kwamba Kanisa linafafanua tu kuwa siku ya Bwana ni Jumapili, lakini profesa wa Chuo Kikuu cha Wasabato cha Andrea [Andrews University] – Samuele Bacchiocci – anaendesha “Semina za siku ya Bwana” katika makanisa yote ya SDA, na ameandika kitabu kiitwacho “From Sabbath to Sunday.” Katika kitabu hiki anaelekeza Jumapili kama siku ya Bwana zaidi ya mara 50 katika kurasa 160 za kwanza!


     Je, nini habari ya Sabato kuwa alama na muhuri wa Mungu?
     “…Sabato ni muhuri wa upendo wetu na kushikamana na Baba mwenye upendo wa mbinguni.” Robert Folkenberg, “Adventist Review,” May 5, 1994, ukr. 18.

     Pasipo kuficha uongozi wa SDA umetupilia mbali Sabato, na wanaongoza washiriki wao kuelekea katika ibada ya Jumapili.

     Nini juu ya habari ya kukosekana ukweli wa kuunga mkono badiliko la ibada kwenda Jumapili?
     “Nini ambacho Waadventista Wasabato wanaamini? Msikie mchungaji/mwinjilisti Jere Webb anavyoona na kuleta ‘Ukweli’ wa sasa. Masomo yanaunganisha…‘Sababu za Kikristo za kuabudu Jumapili’…” “Pacific Union Recorder,” Juni 4, 1990, ukr. 27.

     Je, habari gani kuhusu kutunza Sabato ikiwa tunahitaji kuingia mbinguni?
     “Kama huabudu siku ya Sabato, unakwenda jehanamu? Hasha!” Mwinjilisti wa SDA Kenneth Cox akiwakilisha Kanisa la SDA katika mazungumzo katika luninga yajulikanayo kama “Central Florida Live,” yaliyodhaminiwa na George Crossley, Central Florida, U.S.A. TV Station WTGL, channel 52, Februari 8, 1993.

     Je, nini habari ya Uhuru wa Dini ukiwa ni haki iliyotolewa na Mungu kujifunza, kusimamia, na kutangaza ukweli wake tu, na kuweka wazi maovu?
     “Ikiunganishwa katika mijadala hiyo yamekuwepo mambo yanayohusiana na dhana za kitheolojia kama asili ya Yesu, asili ya mwanadamu, asili ya dhambi, ukamilifu wa tabia, na hoja ihusuyo uwezekano wa Mkristo kuishi maisha yasiyo ya dhambi. Katika kuamua mambo haya magumu ya kitheolojia na kibiblia, si rahisi kabisa kupatiwa ufumbuzi ili kufurahi katika wokovu utolewao kwa neema kwa njia ya imani katika Kristo…Itakuwa ni vema kama tutajiepusha wenyewe kuleta hadharani mambo ya mada hizi na vitu vinavyoleta mabishano katika theolojia ya haki kwa imani….
     “Tunapaswa sote kutafuta namna ya kuhafifisha gharika ya mikanda ya cassette, vijuzuu, vitabu, na vitu vyovyote…Hii ilimaliza mjadala kwa sababu sauti ya mamlaka ya juu ilikuwa imesema.” “Adventist Reviw,” May 24, 1979, ukr. 4-5.

     “Ni wajibu wetu kujifunza Maandiko sisi binafsi, kuomba uongozi wa Roho Mtakatifu, kusalimisha uelewa wetu kwa wale walio Kanisani ambao wana uwezo kuamua mambo tuliyoyagundua, na kisha kwenda sawa na maamuzi ya Kanisa…” “Adult Sabbath School Quarterly,” Lesson 13, Machi 28, 1987, ukr. 92.

     “Uongozi wa Kanisa utaongoza kwa upendo na uelewa, na wafuasi watauunga mkono bila kusita, hata kama kuna mambo mengine katika maamuzi ya uongozi ambayo si mazuri.” “Adventist Review,” Oktoba 25, 1979, ukr. 14.

     “…nafasi ya kundi kubwa la uongozi usiotumia akili ambao umedhamiria kupunguza kasi ya washiriki wanaotafuta kushikilia maoni yasiyoendana na uongozi unaohusika katika dhehebu.” “Eternity magazine,” Septemba, 1957, ikinukuliwa misimamo iliyotamkwa ya viongozi wa Kanisa la SDA; makala yenye kichwa “Je, Waadventista Wasabato ni Wakristo?”

     Si mambo haya haya tu, lakini Kanisa la SDA huwafuta ushirika wale wanaohubiri kwa nguvu ukweli na kuyaweka wazi maovu yaliyomo Kanisani. Pia Kanisa la SDA kule Australia liliwafungulia mashtaka mahakamani Waadventista kadhaa kwa kusambaza Ujumbe (asilia) wa Malaika Watatu katika mtindo wa gazeti katika nyumba zaidi ya 400,000 katika Australia.  Gazeti linaitwa “The Protestant” (See Vital Truths, Issue #12, 1992, P. O. Box 234, Merlin, OR. 97532).

     Je, nini habari juu ya Mnyama ukiwa Ukatoliki wa Kirumi, pamoja na msingi wa Kanisa hili ulio Ekaristi Takatifu, na papa na mfumo wa Ukatoliki kama Mpinga Kristo?
     Mnyama hahesabiwi tena kama Ukatoliki, lakini anahesabiwa isivyo kama “bwana wa uongo” (“Adventist Review,” Desemba 31, 1992, ukr. 10), au akiwakilisha “nguvu zinazopinga watu wa Mungu wa siku ya mwisho” (Robert Folkenberg, “Adventist Review,” May 5, 1994, ukr. 18).

     “Mnyama anawakilisha mfumo wa ibada ya ubinafsi…” “The Return of Elijah,” ukr. 72.
     Je, nini habari juu ya Ekaristi Takatifu ikiwa makufuru na kutukana mbingu?
     “Kusudi la maelezo haya, awali ya yote, ni kuonyesha jinsi uelewa wa Kanisa la Waadventista Wasabato ulivyo kuhusu ekaristi au meza ya Bwana…[na] kukazia uelewa wa Kiadventista na desturi ya ekaristi
     “Katika kujiandaa kwa kusherehekea Ekaristi Waadventista Wasabato hufanya tendo la kuoshana miguu…” “Churches Respond to BEM,” [Baptism, Eucharist, and Ministry], vit 2, ukr. 341-343, 1985. (Hili ndilo jibu rasmi la Kanisa la SDA katika mkutano wa Ekumene ambao walikuwa sehemu katika Mkutano huo ujulikanao kama “Faith and Order Conference of the World Council of Churches (WCC),” Januari, 1982 kule Lima, Peru.)

     Ekaristi pia inaitwa na Kanisa la SDA kama “kiini cha sherehe ya Kanisa la Kikristo” (“BEM,” vit 2, ukr. 341). Kanisa pia linafafanua: “Wakati mwingine Waadventista Wasabato huona ekaristi kama sakramenti” (“BEM,” vit 2, ukr. 342). Pia hueleza kwamba Wasabato “wanauelewa utakatifu wa sherehe ya ekaristi” (“BEM,” vit 2, ukr. 342).
     Hatimaye linaonekana tamko hili la kushangaza:
     “Na tungeendelea kama nafasi ingeruhusu – kutaja misisitizo ya WCC…ya Roho Mtakatifu na Ekaristi. Misisitizo hii yote inaingia vema upana wa ujumbe wa malaika watatu.” “Adventist Review,” May 2, 1991, ukr. 10.

     Je, nini habari juu ya onyo kupinga Mnyama au Ukatoliki?
     “Ingawa ni kweli kwamba kulikuwepo na kipindi katika historia ya Kanisa la Waadventista Wasabato wakati dhehebu lilipochukua msimamo pekee wa kupinga mawazo ya Wakatoliki wa Kirumi…mtizamo huo kwa upande wa Kanisa ilikuwa ni upinzani wa upapa ulioenea katika madhehebu ya Kiprotestanti mwanzoni mwa karne hii na mwishoni mwa karne iliyopita, na ambao sasa umewekwa katika upande wa takataka zilizolundikana kulingana na Kanisa la Waadventista Wasabato linavyohusika.” “EEOC vs PPPA,” Civ #74-2025 CBR, Reply Brief for Defendants,” ukr. 4.

     “…kazi yetu si kulikashifu Kanisa Katoliki la Roma.” “Pacific Union Recorder,” Februari 18, 1985, ukr. 4.
     Je, ni habari gani iliyopo kuhusu Papa kuwa Mpinga Kristo?
     “…kama angefundishwa kwamba Papa ni Mpinga Kristo, nadhani hii ingekuwa kutoelewa. Sidhani kwamba hili ndilo sisi kama Kanisa tunaamini….
     “…[Mpinga Kristo], huyo siyo mtu. Huyo si mtu…” Kenneth Cox, “WTGL TV Interview,” Februari 8, 1993.

     Je, habari gani kuhusu Ukatoliki kama mfumo wa Mpinga Kristo?
     Mpinga Kristo haelezwi kama “upapa,” kwa sababu Kanisa Katoliki “limetetea imani katika asili ya mwili ya Kristo” (“Adventist Review,” Oktoba 27, 1983, ukr. 7). Lakini Mpinga Kristo ameelezwa kuwa:
     – “wakristo walioasi” (“Signs of the Times,” Septemba, 1990, ukr. 25).
     – “mtizamo wa mawazo” (“Signs of the Times,” Septemba, 1990, ukr. 26).
     – wale wanaofundisha “mafundisho ya uongo wanatimiza kigezo hiki” (“Adventist Review,” Oktoba 27, 1983, ukr. 7).
     – wale “wanaotuvuta sisi mbali kutojitoa kwa Kristo” (“Signs of the Times,” Septemba, 1990, ukr. 26).
     – “wale wanaokataa kwamba Yesu ni Kristo au Masia” (“Signs of the Times,” Septemba, 1990, ukr. 25). [Hvyo, Shetani na malaika wake hawawezi kuwa wapinga Kristo pia (Mt 8:29; Mk 1:24; Lk 4:34)!].

     Je, nini habari ya Mnyama mfano wa Mwanakondoo akiwa Marekani?
     Mnyama mfano wa Mwanakondoo haelezwi kama Marekani, lakini anaelezwa visivyo kama “mamlaka inayofanyiza sanamu” (“Adventist Review,” Oktoba 15, 1992, ukr. 10). Au imeelezwa kama “kumpinga roho” (“Adventist Review,” Septemba 7, 1989, ukr. 22-23).


     Je, nini habari juu ya Sanamu ya Mnyama yakiwa ni mafundisho ambayo Makanisa ya Kiprotestanti na Baraza la Umoja wa Makanisa [WCC] hukubaliana bila hitilafu; yatakayopelekea Makanisa yote kuungana katika jukwaa la kile wanachokiamini pamoja katika Kristo, na kutumia serikali kuyasaidia katika kuchukua hatua kutokana na makubaliano yao?
     Sanamu ya Mnyama haijaelezwa kama Uprotestanti ulioasi, bali imeelezwa visivyo kama sanamu au sura ya kitu tunachokiabudu “kuliko Mungu Muumbaji” (“Adventist Review,” Oktoba 15, 1992, ukr. 9).
     Sanamu ya Mnyama pia inaelezwa kama kujiweka “mwenyewe juu kinyume na Bwana wa mbinguni…aina hii ya sanamu” (“Adventist Review,” Oktoba 15, 1992, ukr. 10).

     “…Sanamu ya Mnyama ni kulazimisha wajibu wa kidini kwa kutumia mamlaka ya binadamu….Muungano wa imani kwa Mungu…na kujaribu kutii kwa juhudi zako mwenyewe, ndiyo Sanamu ya Mnyama.” “The Return of Elijah,” ukr. 77.

     Nini habari ya Sanamu ya Mnyama kusimamishwa wakati Makanisa yote yanapounganika, na Serikali inayaunga mkono na kulazimisha makubaliano yao?
     “Kama yeye [mnyama mfano wa Mwanakondoo au mpinga roho] hawezi kutuongoza sisi kwenye uasi wa wazi (ambao unatupatia sisi alama katika vipaji vyetu vya uso), basi hutuongoza kupokea kijialama (au sura ya juu juu) cha utii (kinachotuwezesha sisi kupokea alama katika mkono.
     “Hivi ndivyo ambavyo mpinga roho anavyofanya sanamu ya mnyama. Utii wa juu juu, ambao haujajikita katika upendo, hatimaye utatoa tabia kama ile ya mnyama.” “Adventist Review,” Septemba 7, 1989, ukr. 23.

     Je, ni nini habari juu ya onyo dhidi ya Sanamu – au Makanisa ya Kiprotestanti, ikiwa ni pamoja na Baraza la Umoja wa Makanisa (WCC)?
     Kanisa la SDA halionyi juu ya hatari inayokuja kwa Makanisa ya Kiprotestanti yaliyoasi au Baraza la Umoja wa Makanisa [WCC], kwa sababu yameunganishwa nalo na ni sehemu yake kwa njia ya fundisho la Utatu Mtakatifu!
     Mwaka 1973 Kanisa la SDA, Kwa kushirikiana na Umoja wa Makanisa, liliandika kitabu kiitwacho “So Much in Common.” George Vandeman pia aliandika kitabu, mwaka 1986, kikisifia Makanisa yaliyoasi kiitwacho “What I Like About...The Lutherans, The Baptists, The Methodists, The Charismatics, The Catholics, Our Jewish Friends, The Adventists; Rescuers of Neglected Truth” kilichochapwa na Pacific Press Publishing Association, 1986.
     Kwa hiyo Kanisa la SDA halijajitenga kutoka Babeli, bali limeungana kikamilifu nao.
     “…tunapendana sisi kwa sisi [Wakristo wa madhehebu mengine], na tunafanya kazi pamoja. Hii ndiyo jumla ya yote….Hiki ndicho sisi [Kanisa la SDA] tupo duniani kukifanya – ni kufaidika kutoka kwa kila mmoja wetu [madhehebu mengine].” Kenneth Cox, “WTGL TV Interview,” Februari 8, 1993.

     Kanisa la SDA pia ni sehemu ya Baraza la Kitaifa la Umoja wa Makanisa (NCC) na Baraza la Umoja wa Makanisa (WCC) (Andika katika anuani iliyo juu ili kupata rejea hizi). Lakini kauli ifuatayo ingewasaidia Waadventista kutambua kwamba hii ni kweli:
     “Waadventista Hupata Marafiki Katika Umoja wa Makanisa” “Canadian Union Messenger,” Septemba, 1983, ukr. 5.

     Je, ni habari gani juu ya Alama ya Mnyama, ikitolewa kwa wale wanaoabudu siku ya Jumapili baada ya kuwa imekuwa sheria, wakati ukijua kwamba siyo Sabato ya Mungu, na kwamba hatupaswi kutii mamlaka ya kiserikali kuhusiana na amri hii?
     “Kanuni ya Alama ya Mnyama ni kwamba mwanadamu anaweza…kufanya chochote ambacho kitamfikisha mbinguni na kumfanya akubalike kwa Mungu.” “Marked,” ukr. 88.

     “Alama ya Mnyama huhusisha…wokovu kwa matendo ya sheria.” “The Return of Elijah,” ukr. 73.

     “…Alama ya Mnyama, ambayo ndiyo wokovu kwa matendo ya sheria ya haki ya mtu binafsi.” “Marked,” ukr. 38.

     Je, nini habari ya kupokea Alama ya Mnyama ikiwa tutatii mamlaka ya kiserikali na kupiga magoti kwa amri ya Jumapili?
     “Ellen White...[akiandika juu ya amri za Jumapili] aliwaambia watu wasiende kinyume na mamlaka ya serikali.” Kenneth Cox, “WTGL TV Interview,” Februari 8, 1993.

     Na kama hii haikutosha, Kanisa la SDA linafundisha kwamba Alama ya Mnyama si ibada ya siku ya Jumapili, bali humaanisha ibada ya siku ya Sabato!
     “…Sabato…[ni] alama ya utii kwa Mungu….Lakini tunapaswa kuwa na tahadhali! Mtu yeyote ambaye mlengo wake ni kwenye Sabato…ambaye anaangalia katika utunzaji wake wa Sabato kama kigezo cha wokovu wake…ni mtahiniwa wa alama ya mnyama.” “Adventist Review,” Septemba 7, 1989, ukr. 26.

     Je, ni habari gani juu ya habari ya roho kutokufa, kwamba kuna kaburi tu la kupumzika pindi tunapokufa, lakini hakuna jehanamu tunaposhuka; na zawadi ya kutokufa itatolewa tu Yesu ajapo mara ya pili?
     Biblia hufundisha kwamba “roho itendayo dhambi, itakufa” (Eze 18:20). Lakini Kanisa la SDA hufundisha kwamba hakuna yeyote anayeweza kushinda dhambi zote, na bado Mungu hawezi kukuangamiza, bali atakufanya mkamilifu na kukuchukua mbinguni kukupatia uzima wa milele bila shida. Hiyo ndiyo roho kutokufa!
     “…Lazima mara nyingi nisifikie jitihada zangu….Wale walio na njaa na kiu ya haki…wanakazania lengo gumu…” “Adventist Review,” Desember 6, 1984, ukr. 6.

     “…hatuwezi kuishi bila kutenda dhambi.” “The Return of Elijah,” ukr. 95.

     “Tu wadhambi. Tutakuwa wadhambi mpaka Yesu ajapo, na wadhambi kamwe hawawezi kutoa utii….Yote tunayoweza kuyafanya ni kuachilia mbali tumaini la kuwa na utii halisi.” “Faith That Works,” ukr. 175.

     “…ikiwa tunakufa katika kutenda dhambi wakati tunapoongoka, tutatenda dhambi tena? Tutaendelea kutenda dhambi kama Wakristo – si kwamba tunapenda, lakini kwa sababu tu binadamu.” “VOP News,” May, 1985, ukr. 2-3, H.M.S. Richards, Jr.

     “Tunatakiwa kukumbuka kwamba ni pale tu Yesu atakapokuja ndipo tutafanywa wakamilifu.” “Ministry,” Desemba, 1965, ukr. 9.

     Udanganyifu wa kinachodhaniwa kuwa ukweli juu ya roho kutokufa, wa kuendelea katika dhambi mpaka Yesu ajapo na bado mtu asiangamizwe bali afanywe kuwa mkamilifu, umetumika Kanisani katika mwendelezo wa uasi na kukataa ukweli wa Mungu.
     “…Kanisa la masalio la Mungu ni Laodikia ambalo bila shaka lina matatizo yake. Lakini hakuna uhakika kamili wa Mungu kutoa tiba…Ahadi ambayo Kristo atakapokuja ‘atajiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lolote kama hayo.’” “Adventist Review,” Machi 7, 1991, ukr. 10.

     Nini habari ya kwamba kuna kaburi tu, lakini hakuna jehanamu ya kwenda?
     “…[na] Kanuni ya Mitume, hufafanua: ‘Naamini katika Mungu Baba…na katika Yesu Kristo Mwanae wa pekee, Bwana wetu, ambaye…aliteswa chini ya mamlaka ya Pontio Pilato, alisulubishwa, akafa, na kuzikwa. Alishuka kuzimu, na siku ya tatu akafufuka tena kutoka kwa wafu, akapaa mbinguni…’
     “Kwa kukiri huku…ambako kwa kanuni kunaturejesha katika karne ya pili B.K., Mkristo wa Kanisa la Waadventista Wasabato anaweza kusema kwa moyo wote, ‘Amina!’” “Adventist Review,” Juni 10, 1982, ukr. 4 (msisitizo ni wa awali).

     Je, ni nini habari ya zawadi ya kutokufa pale tu Kristo ajapo?
     “Biblia huleta uzima wa milele kama zawadi ya wokovu ya sasa….Siyo baadaye tu, lakini sasa.” “Signs of the Times,” May, 1992, ukr. 11 (msisitizo ni wa awali).

     “Uhusiano wetu mpya na Kristo [kuzaliwa tena] huja na zawadi ya uzima wa milele.” “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 124).

     “Kama tukikubali injili yake [Kristo] na kuamini kuwa Baba yuko kama alivyomwakilisha, tayari tumeishaingia katika uzima wa milele.” “Adventist Review,” Oktoba 8, 1992, ukr. 9.
(Kauli nyingine inayofanana na hii angalia “Adventist Review,” August 11, 1983, ukr. 7.)


     Ikiwa kweli tunao uzima wa kutokufa milele sasa, basi hatuna tena asili ya kuanguka katika dhambi, lakini tutakuwa na asili takatifu ya kutoanguka – au miili mitakatifu! Fundisho hili la uongo lilianza kwenye karne ya 19, na Ellen White alionya kwamba lingerudiwa tena muda mfupi kabla mwisho haujaja (“Selected Messages,” kitabu cha 2, ukr. 36).

     Je, ni kweli kwamba Kanisa la SDA linafundisha juu ya miili mitakatifu?
     “…tunazaliwa na asili ambayo hufurahia kufanya dhambi zaidi ya kutofanya dhambi. Hivyo tunahitaji asili mpya….Hicho ndicho Yesu anachokitoa. Ameahidi kubadilisha asili zetu ikiwa tutamruhusu.” “Signs of the Times,” Juni, 1992, ukr. 20.

     “…Yesu alituchukua sisi katika mikono yake ya baraka na akatununulia sisi asili mpya kabisa, uzima mpya ambao anatupatia…” “VOP News,” Februari, 1976, ukr. 7, H.M.S. Richards, Jr.

     Je, ni nini habari ya hasira ya Mungu ikiwa ni mapigo saba ya mwisho?
     “Malaika wa tatu wa Ufunuo 14 huonya kuwa mwishoni hasira ya Mungu, isiyochanganywa na rehema, itamwagwa juu ya vichwa vya wanadamu wasiotubu…. Mungu anawaacha watu kama hao na anawageuza ili wapokee matokeo ya uasi wao….Kwa sababu imani na upendo havilazimishwi, Mungu atafanya kitu gani zaidi kwa huzuni kuwaacha hao wanaomkataa?
     “Hasira ya Mungu…ni kuwaacha kwa upendo katika kukatishwa tama wale wasiomtaka Yeye, hivyo akiwaacha kukabiliana na madhara yasiyoepukika ya uchaguzi wao wa uasi.
“Hii [ndiyo] picha ya hasira ya Mungu…” “Signs of the Times,” July, 1978, ukr. 19.

     Je, ni nini habari ya Hema Takatifu ya mbinguni ikiwa na vyumba viwili – patakatifu na patakatifu mno?
     “Kuna Hema Takatifu mbinguni...Ndani yake Kristo anahudumu kwa ajili yetu...Mwaka 1844, mwishoni mwa kipindi cha unabii cha siku 2300, aliingia awamu ya pili na ya mwisho ya huduma yake ya upatanisho.” “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 312, #23.

     Kauli hii inaondoa maneno “mahali patakatifu mno” ambayo yalitumiwa katika kauli zingine za misingi ya imani ya Kanisa la SDA (1872 #10; 1912 #10), na kuingiza badala yake maneno “awamu ya pili ya mwisho” (Makala nyingine ambayo haitaji vyumba viwili wakati wa kujadili Hema Takatifu ya Mbinguni: “Adventist Review,” Februari 16, 1984, ukr. 7-8).

     Je, ni nini habari ya kazi ya Kristo ya upatanisho unaoendelea katika patakatifu pa patakatifu (chumba cha pili cha Hema ya Mbinguni) ambayo ilianza tu baada ya Oktoba 22, 1844 mwishoni mwa siku 2300, na haina mwisho mpaka atakapomaliza kazi yake kabla ya kuja mara ya pili?
     “…tendo la kafara ya pale msalabani – iliyomalizika, kamili, na upatanisho wa mwisho kwa dhambi ya mwanadamu….Huo ndiyo uelewa wa Waadventista juu ya upatanisho…” “Ministry,” Februari, 1957, ukr. 10, 44.

     “…Tendo la Upatanisho lilikamilishwa pale msalabani…” “Movement of Destiny,” ukr. 505 [msisitizo wa awali]).

     “Upatanisho umekamilishwa…” “Adventist Review,” Februari 16, 1984, ukr. 7.

     “Upatanisho, au kuondoa uhasama, kulimalizika pale msalabani…na mdhambi aliyetubu anaweza kuamini katika kazi iliyomalizwa na Bwana wetu.” “Seventh-day Adventists Believe…” ukr. 315.

     “Leo Waadventista Wasabato wanafundisha kwamba kafara ya upatanisho ilifanyika msalabani. Lakini waasisi wetu kwa ujumla hawakuamini kwamba upatanisho ulifanyika pale msalabani.” “The Sanctuary and the Atonement,” ukr. 586, Kilichopitishwa na The Biblical Research Committee of the General Conference of Seventh-day Adventists na kuchapwa na Review and Herald Publishing Association, 1981.
(Kauli zingine zenye mtiririko wa mawazo haya ni: “Adventist Review,” Nov 6, 1986, ukr. 18, Januari 6, 1983, ukr. 3, Feb 7, 1985, ukr. 9, Machi 5, 1992, ukr. 11 (251); “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 106. )

     Msimamo huu mpya ulikuwa kinyume kabisa na maandiko mengi ya waasisi na Shuhuda zinazohusu ukweli katika jambo hili. Kwa hiyo ili kutibu kipingamizi hiki, Kanisa lilichapa kauli hii:
     “Kwa hiyo, pale mtu anaposikia Msabato anasema, au kusoma katika vitabu vya Kisabato – hata katika maandiko ya Roho ya Unabii (Ellen G. White) – kwamba Kristo anafanya upatanisho sasa, inapaswa kueleweka kuwa tuna maana kwamba Kristo sasa anatumia faida za kafara ya upatanisho aliyoifanya msalabani.” “Questions on Doctrine,” ukr. 354-355.

     Kutokana na kwamba Kanisa la SDA limebadilisha huu ukweli juu ya upatanisho, na linafundisha kwamba ulikamailika pale msalabani, lazima washughulikie mada ya kwamba ni kuhani tu anayeweza kufanya upatanisho. Kristo hakuwa kuhani hapa duniani (Ebr 8:4), na hivyo upatanisho usingeweza kufanyika pale msalabani.
     Lakini Kanisa la SDA hufundisha nini kuhusu jambo hili?
     “…wakati wa huduma ya duniani Kristo alikuwa kuhani na kafara pia. Kifo chake msalabani ilikuwa sehemu ya kazi yake ya kikuhani.” “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 53.

     Je, ni nini habari ya Kristo kama Kichwa au Mchungaji wa kwanza wa Kanisa lake, Kuhani wetu mkuu, na Mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu?
     “Mchungaji Robert H. Pierson ni Rais wa Baraza Kuu la Waadventista Wasabato na, kama ilivyo ni mchungaji wa kwanza wa Kanisa la Waadventista Wasabato….Ikiwa ni pamoja na mimi kama mchungaji wa kwanza.” “EEOC vs PPPA,” Civ #74-2025 CBR.

     Sasa ikiwa mchungaji wa kwanza au kichwa cha Kanisa la SDA siyo Kristo, lakini Rais wa Baraza Kuu, basi ni nani kuhani wetu mkuu au mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu?
     “Tunaona hapa kwamba wajibu wake mkuu [Aron] ulikuwa ni kufanya kazi kama mpatanishi, kama kiungo kati ya watakatifu na najisi, kati ya Mungu na mwanadamu….Hali kadhalika mchungaji [SDA] wa injili leo ni kuhani mkuu....Leo sisi [wachungaji wa SDA] ni makuhani wakuu….Ni jukumu kuu kiasi gani kutumika kama wapatanishi kati ya Mungu na mwanadamu!” “Ministry,” Desemba, 1961, ukr. 27, 29.

     Je, ni nini habari ya Kanisa la kweli la Mungu likiwa limeanzishwa na kusimikwa katika Kristo na ukweli wake, na alama zote za Kanisa la kweli zilizoorodheshwa katika Ufunuo 12:17 na 14:12; ambazo ni “kushika amri za Mungu,” “imani ya Yesu” na “ushuhuda wa Yesu” au “roho ya unabii” katika Ufunuo 19:10 ikiwa ni maandiko ya Ellen G. White; na hivyo maandiko haya yakiwa na kusudi lake endelevu, na kwamba bado yanapaswa kufuatwa leo?
     “Alama nne kimadaraja za Kanisa la Kibiblia zinaendana na Kanisa la Waadventista Wasabato: utakatifu wake (katika Yesu Kristo), ukatoliki wake (kuenea ulimwenguni pote), utume wake (sawa na ushuhuda wa mitume/waanzilishi), umoja wake (Bwana mmoja, Imani moja, Ubatizo mmoja).” “Adventist Review,” Oktoba 1, 1992, ukr. 27 (msisitizo wa awali).

     Kwa hiyo Kanisa la SDA linathibitisha ukamilifu wake kuwa ni Kanisa la Mungu la kweli Kibiblia leo, si kwa kutunza amri za Mungu au kwa kufuata Roho ya Unabii, lakini kwa kuwa takatifu, Katoliki au kuwa katika ulimwengu wote, la mitume, na moja au lililoungana. Kwa nini hii ni muhimu? Kwa sababu kwa miaka mamia Kanisa Katoliki limedai kuwa na alama hizo hizo nne kuyakinisha kwamba ndilo Kanisa la kweli la Mungu Kibiblia!
     “Kuna Alama Nne ambazo kwazo Kanisa la Kristo [Katoliki] linaweza kutambuliwa. Linapaswa kuwa Moja, Takatifu, Katoliki, na la Mitume.” “Converts Catechism of Catholic Doctrine,” ukr. 26, na Peter Geiermann (see also “The Catholic Encyclopedia,” ukr. 99).

     Hakika, Kanisa la SDA linafanana na Ukatoliki wa Kirumi, na linapaswa kuunganishwa kama sehemu ya Sanamu ya Mnya ma – au Makanisa yale ya Kiprotestanti yaliyo na sura ya Ukatoliki wa Kirumi! Kwa uhakika, Kanisa la SDA lina sura au ni sanamu ya Roma karibu zaidi kuliko Kanisa lolote la Kiprotestanti katika Marekani!
     Jaji William T. Hart wa Mahakama ya Wilaya, Wilaya ya Kaskazini ya Illinois, Kanda ya Mashariki, alitoa uamuzi kupendelea Baraza Kuu la Waadventista Wasabato ambao walikuwa wanashtakiwa na Derrick Proctor. Jaji Hart alieleza:
     “Vielelezo vya Kanisa ambavyo vinaeleza muundo wa Kanisa na serikali yake vinathibitisha kwamba sehemu zote za Kanisa ni sehemu za kitu kimoja. Kufuata Kanisa la Kikatoliki la Kirumi, Kanisa la Waadventista limeweka mambo yake katika serikali kuu [centralization] kuliko madhehebu ya Kikristo katika nchi hii.” “Derrick Proctor vs General Conference of SDA, case #81 C 4938, Findings of Fact, Section B, Church Objectives and Structures,” ukr. 22, Oktoba 29, 1986.

     Je, ni nini habari ya kufuata maandiko ya Ellen G. White ya Roho ya Unabii leo?
     “...[vitabu 9 viitwavyo ‘Testimonies for the Church,’ ambavyo ni matokeo ya shuhuda za watu] ulikuwa ni ujumbe maalum kwa huyo mtu ambao kwa jumla hauwezi kutumika kwa kila mtu….Kwa hiyo huwezi kuchukua shuhuda na kuzifanya matumizi hayo ya jumla kwa kila mtu….[Kwa hiyo wakati] Mungu alipoongea kwake…na hiyo haina maana kwamba maneno hayo hayawezi kutumika kwa kila  mtu..” Kenneth Cox, “WTGL TV Interview,” Februari 8, 1993.

     “Maandiko ya Ellen White yalikuwa na makusudi yake…” “Angry Saints,” ukr. 108.

     Je, ni nini habari ya Haki ya Kristo ikituwezesha sisi kukubalika tena kwa Mungu, kupokea neema yake ambayo hutusaidia kushinda dhambi zote na kukamilisha utakatifu kabla ya ujio wa Kristo; kwamba sheria ya Mungu bado inatufunga leo, na Kristo kuitunza hakutuweki huru sisi kutoitunza pia; utakaso au kukamilika siyo hapo hapo, lakini ni tukio la taratibu katika maisha yetu yote wakati tukipambana na kuelekea juu katika mstari ulionyooka na mwembamba kwenda mbinguni; hivyo wakati tukiwa duniani, hakuna aliyeokolewa, au anaweza kusema au kuhisi kwamba ameokolewa mpaka atakapokuwa mbinguni; na kwamba vazi la haki ya Kristo halitaweza kufunika uovu wowote wala dhambi ambayo haijaungamwa – hivyo hakuna ambaye anaweza kupata wokovu katika Yesu wakati akiendelea na dhambi?
     “Wengi wanaamini kimakosa kwamba kusimama kwao mbele za Mungu kunategemea kazi zao nzuri au mbaya.” “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 121.

     “…[tunapaswa] kutupilia mbali wazo kwamba tunaweza kuwa na utii mkamilifu.” “Faith That Works,” ukr. 168.

     “Utii mara zote ni kwa imani tu…si kwa juhudi zetu wenyewe.” “Obedience of Faith,” ukr. 88.

     Ni nini ambacho Kanisa la SDA linaamini juu ya kushinda dhambi zote?
     “…Yeye [Mungu] hatutegemei sisi kushinda dhambi.” “Salvation By Faith,” ukr. 71.

     “Inasulubisha kukiri kwamba hatuwezi kushinda dhambi, kwamba hatuwezi kutii, kwamba hatuwezi kutoa haki, lakini kwamba Yesu lazima afanye haya yote kwa ajili yetu.” “Faith That Works,” ukr. 172.

     “Hatutafikia ukamilifu wa kutotenda dhambi katika maisha haya.” “Review,” May 19, 1966, ukr. 4.

     Ni nini ambacho Kanisa la SDA huamini juu ya kufanya kazi na Mungu ili kushinda dhambi na kuishi maisha ya haki – kuendelea kupigana na kupanda juu katika njia iliyonyooka na nyembamba iendayo mbinguni?
     “…Mungu hajawaita viongozi kutoa picha kamili, isiyo na mawaa ya Yesu…” “Church Ministries Worker: A Journal for Church Leaders,” Januari-Machi, 1987, ukr. 4, lililochapwa na Pacific Press Publishing Association.

     “Mungu tayari ameshinda nguvu za dhambi. Hatutakiwi kupigana tena na tena ili kushinda dhambi. Hii ni kwa sababu Yesu tayari amefanya hili, mara moja kwa ajili ya wote pale msalabani….Je, ni kitu cha kudhania kuwa ni kweli kwa upande wetu kujaribu kushinda dhambi ‘tena’ katika maisha yetu?…Dhambi ni kubwa sana na ina nguvu kwa upande wetu kutupoteza sisi wenyewe kwa jinsi hiyo….Haijalishi ni nini, tutaendelea kufanya dhambi kwa sababu tu sisi ni wadhambi….Tukiwa tumekubali kwamba, hata kama, hatutakiwi kuangalia yote yamefanyika juu ya kutofaulu kushinda dhambi.” “Cornerstone Connections Youth Quarterly,” ukr. 60-62, 65.

     “Matendo ya haki ni dini ya jinsi ya mwilini, na siku zote imekuwa….Siyo mapenzi ya Mungu kwamba tufanye njia yetu kwenda juu ya mlima mkali wa mbinguni, wa damu na huku tumenyenyekea, tusiokuwa na uhakika kama tutafika au la.” “Adventist Review,” Oktoba 8, 1992, ukr. 9.
(Kauli nyingine inayofanana na hii angalia “Adventist Review,” Machi 2, 1989, ukr. 10).

     Ni nini ambacho Kanisa la SDA huamini juu ya sheria ya Mungu kwamba bado inatufunga leo, na Kristo kuitunza hakutuweki sisi kutoitunza kamwe?
     “…[dhana potofu ni kwamba] tunapaswa kufanya jambo ili kujiokoa wenyewe kutoka dhambini. Ni roho [mchafu] ambaye hufundisha kwamba hatuwezi kutumaini yote kwa Kristo, na kumwacha afanye yote kwetu kwa ajili ya haki yetu.” “Angry Saints,” ukr. 47.

     “...tumewekwa huru na sheria…[Roho] humweka huru muumini kutoka katika sheria…na kutimiza matakwa ya haki ya sheria ndani yake.” “Adventist Review,” Novemba 17, 1983, ukr. 7.

     “Sheria imechukuliwa kabisa. Imechukuliwa juu yake [Yesu], kwa hiyo niko huru.” “Adventist Review,” Aprili 6, 1989, ukr. 13.
(Kauli nyingine inayofanana na hii angalia: “Adventist Review,” Januari 2, 1986, ukr. 13, Aprili 18, 1985, ukr. 17.)

     Je, ni nini juu ya utakaso au kukamilika kukiwa siyo kitu cha hapo hapo, lakini kukiwa ni tendo la kuendela katika maisha yetu yote?
     “Na juu ya maisha yaliyopita ya muumini, wakati wa kuhesabiwa haki muumini anatakaswa pia.” “Seventh-day Adventist Believe…,” ukr. 123.

     “…ukamilifu [katika Kristo]…unaendana, au unadhaniwa, kadiri ambavyo inategemeana na uhusiano unaotakiwa na Kristo. Unapatikana hapo hapo kwa tendo la akili la utashi kukubali haki ya Kristo inayowekwa na kutolewa, na inahifadhiwa maisha yote isipokuwa mtu akikataa kuwa na uhusiano na Kristo….Anahesabiwa kuwa kamili mbinguni, si kwamba huwa hafanyi makosa, lakini kwa sababu, pamoja na makosa, Mungu humhesabia haki kwa njia ya haki kamili ya Kristo. Kujiweka wakfu kusiko na mipaka kuhusu lengo, kutolegea katika kulitimiza, ndiyo tu matakwa ya Mungu.” “Review,” Juni 10, 1965, ukr. 12.

     Je, ni nini habari ya kwamba hakuna yeyote anayeweza kusema au kuhisi kwamba ameokolewa kabla ya kuingia mbinguni?
     “Je, unashangaa kama umeokolewa?...Je, unaamini kwamba Yesu ni mwokozi wako? Umeungama dhambi zako? Je, umejitoa mwenyewe kwake? Basi, bila kujali vile unavyohisi – iwe unajisikia ‘vizuri’ au la – umeokolewa….Ni watu waliookolewa tu …wanajua jinsi wanavyoshindwa kufikia kiwango cha Mungu….[Yeyote] ambaye anampenda Yesu anajua na anaweza kujua kwamba ameokolewa.” “Signs of the Times,” Juni, 1989, ukr. 12-14 (msisitizo wa awali).

     Je, ni habari gani juu ya Vazi la haki ya Kristo kwamba haliwezi kufunika uovu wowote au dhambi moja ambayo haijaungamwa.
     “Ukamilifu wa tabia yake (Kristo) unaelezwa kama shela ya harusi au vazi la haki ambalo analitoa kufunika mavazi machafu ya binadamu katika harakati zake za kupata haki.” “Seventh-day Adventists Believe…,” ukr. 114.

     “…Inawezekana kwa Mkristo anayekua kugundua kwamba ana dhambi anayoijua ambayo inaendelea katika maisha yake na wakati huo huo kukawepo na kuendeleza uhusiano na Kristo.” “To Know God,” ukr. 93.

     “…katika watu ambao hawajakamilika kukuzunguka…umeweza kuona vazi la haki ambalo tayari amewafunika.” “Adventist Review,” July 5, 1984, ukr. 3.

     “…[injili ya milele] inajumuisha utii wa haki wa Kristo kusimama mahali pa uovu na uasi wetu, na haki yake isiyo na doa kusimama mahali pa dhambi zetu na uchafu.
     “Hicho ndicho kiini cha ndani cha Injili ya milele. Huo ndiyo msingi pekee wa utakatifu mbele za uso wa Mungu….Ni haki yake, si mafanikio yetu. Hiyo ndiyo Injili katika utenda kazi wa utukufu. Huo ndiyo Ujumbe wa Malaika wa Kwanza, wa Pili, na wa Tatu katika ‘ukamilifu.’” “Movement of Destiny,” ukr. 634 (msisitizo wa awali, toleo la 1971).

     Je, ni nini habari ya mtu kupata wokovu wakati akiendelea katika dhambi?
&n